*Mpaka sasa, Kampuni imechangia zaidi ya $1M za kukabiliana na majanga

TANGU kuanza kwa janga la COVID-19, Meridian Gaming Group, moja ya kampuni kubwa inayojihusisha na michezo ya kubashiri imekuwa ikisaidia jamii kwenye maeneo yote inayofanyakazi. Imekuwa hivyo kwenye maonesho ya G2E, Las Vagas.

Siku ya hitimisha maonesho ya g2E, Meridian Group iliwasilisha matokeo ya mchakato wa kukabiliana na janga la COVID-19 na kuonesha kuwa, ilichangia zaidi ya $1M kwenye miradi inayohusiana na Covid ikiwa ni sambamba na kuyafikia takribani majiji 150 barani Ulaya, LATAM na nchi za Kiafrika.

Wahudhuriaji wa maonesho ya gaming expo walivutiwa zaidi na uhalisia kuwa, Meridian Group ilijitolea vituo vyake vingi kuwa sehemu za kutolea chanjo kwenye maoneo mengi duniani, sio tu kwa wafanyakazi wake bali kwa wananchi wote.

Kwa zaidi ya miezi 18 sasa, Meridian Gaming imeendelea kuzisaidia hospitali za taifa, vituo vya afya, nyumba salama, vituo vya kuongezewa damu, mashirika ya usawi wa jamii, mashirika ya afya yaliyopo Kusini Mashariki mwa Ulaya, Umoja wa Ulaya, LATAM, Amerika ya Kati, Afrika na Asia.

Pia, kampuni kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) walisaidia usambazaji wa chanjo duniani, nafuu ya covid-19 na mpango wa kukabiliana na janga hilo. Shukrani kwa kampuni kama Meridian, WHO iliweza kuzisaidia nchi zilizoathirika zaidi kwenye jitihada zao za kampeni ya kusambaza chanjo ya COVID-19.

Haijawahi kutokea, jamii zetu zimepitia majaribu makubwa na kwa sababu hiyo, Meridian imekuwa mfano wa kutukumbusha ushirikiano kote duniani ni njia sahihi ya kukabiliana na majanga.

Meridianbet, Nyumba Yenye Odds Bora na Bonasi Kubwa!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...