Na Mwandishi Wetu, Ufaransa
JAMHURI ya Muungano wa Tanzania imechaguliwa kuwa mjumbe wa Bodi Tendaji ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kipindi cha mwaka 2021-2025; kwenye Mkutano Mkuu wa 41 wa UNESCO unaoendelea Paris, Ufaransa.
Kwenye uchaguzi huo, uliofanyika Novemba 17,2021 , Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepata kura 160 kati ya 178 zilizopigwa na nchi wanachama. Nchi zingine zilizochaguliwa kutoka kundi la Afrika kuhudumu kwenye bodi hiyo ni Angola, Botswana, Djibouti, Afrika Kusini na Congo.
Pamoja na masuala mengine, Bodi Tendaji inahusika na usimamizi wa utekelezaji wa bajeti ya Shirika kupitia miradi mbalimbali itakayopendekezwa. Hivyo nafasi hiyo itakuwa ni fursa ya kushiriki katika maamuzi ya Shirika hilo kwa kuzingatia mahitaji ya kundi la nchi zinazoendelea.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...