kampuni inayoongoza ya mfumo wa usafiri wa kukodi barani Afrika, imezindua huduma ya Boda-boda jijini Dodoma katika jitihada zake za kurahisisha upatikanaji wa huduma za usafiri nchini Tanzania.

Huduma ya Bolt Boda inawapatia wasafiri njia mbadala ya kusafiri, ikiongeza ukuaji wa huduma za usafiri wa kukodi zinazopatikana sokoni kwa sasa. Huduma hii vile vile inakusudia kuleta huduma za usafiri za uhakika na za bei nafuu za Bolt karibu na wateja wakati huo huo ikiwa inaimarisha upatikanaji wa huduma zake hapa nchini.
 
“Tunaendelea kuongeza wigo wa huduma zetu kwa manufaa ya wateja wetu na kuwekeza rasilimali katika huduma zenye ubora ambazo zinakidhi mahitaji ya jamii. Pikipiki ni moja kati ya njia ya haraka zaidi ya kutoka sehemu moja kwenda nyingine ndani ya jiji la Dodoma, na tunashauku ya kuwapatia wateja wetu njia mbadala na nafuu ya kwenda sehemu mbalimbali ndani ya jiji,” Alisema bwana Remmy Eseka, Meneja wa Bolt Nchini Tanzania.Uzinduzi huu wa huduma ya safari ya Bolt Boda  unaleta mtandao unaokuwa kwa kasi wa usafiri wa Bolt kwa njia ya boda boda kwenye miji mitatu nchini Tanzania ikiwemo Dar es salaam, Mwanza na Dodoma.
 
Kampuni ya Bolt inatoa fursa mbalimbali za huduma za usafiri wa kukodi kwa gharama nafuu sokoni na inaendelea kuwa na ukuaji imara ambao unaendeshwa na mahitaji ya huduma zake za bei nafuu na zenye ubora.
 
Huduma ya Bolt BODA ni huduma nyingine ya nyongeza katika orodha ya huduma mbalimbali inayotolewa na Bolt, ikiwemo huduma ya Bolt Base na Bolt Lite kwaajili ya kuhudumia mahitaji ya kipekee ya wasafiri wa Dodoma.
 
Wateja wanaweza kupata huduma ya Bolt BODA kwa kupitia kwenye App ya Bolt kwa gharama nafuu ya TSZ 1,000. Gharama ya TZS 220 kwa kila kilomita moja, gharama ya TZS 50 kwa dakika na nauli ya msingi ya TZS 600. Madereva wa Bolt watabakiwa na 80% ya mapato yao na bolt itawatoza ada ya asilimia 20% kwa kila safari, ambayo inaweza kulipiwa kwa kadi au fedha taslimu.
 
Kampuni ya Bolt itasajili waendesha boda-boda wenye vitambulisho vya Taifa, leseni ya udereva, cheti cha polisi cha ithibati, leseni ya vyombo vya usafiri LATRA, kadi ya usajili ya gari (usajili wa kibiashara) na bima ya vyombo vya usafiri. (Kibiashara).
 
“Biashara yetu kubwa ni kutoa huduma ya usafiri ya uhakika, salama na ya bei nafuu kwa kila mmoja, na tunashauku ya kufanya huduma ya usafiri iwe rahisi zaidi, ya haraka nchi nzima katika kipindi hiki cha sikukuu”. Alisema Remmy.
Kuhusu Bolt
 
Bolt ni kampuni ya mfumo wa usafiri yenye asili ya Ulaya inayoongoza ambayo imedhamiria katika kufanya usafiri wa maeneo ya mijini kuwa wa gharama nafuu, rahisi na wenye ufanisi.
 
Kampuni ya Bolt ina zaidi ya watumiaji milioni 50 katika zaidi ya nchi 40 katika bara la Ulaya na Afrika. Huduma zake zinajumuisha usafiri wa kukodi, kwa wasafirishaji wadogo wadogo wenye pikipiki ndogo na baiskeli za kutumia umeme pamoja na usafirishaji wa vyakula na vifurushi.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...