Khadija Kalili: Na Khadija Kalili, Chalinze
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani Alhaj Abdul Sharif amewapongeza wadau wa elimu Jimbo la Chalinze huku akitoa rai kwa Halmashauri ya Chalinze kuwaunga mkono katika juhudi zilizoonyeshwa na jukwaa hilo katika kupandisha kiwango cha elimu.
Akizungumza kama mgeni rasmi kwenye Kongamano hilo la lililoandaliwa na wadau wa elimu Chalinze Mwenyekiti huyo alisema kuwa wakati umefika kwa wana Chalinze kujitathimini kwa kina hali ya kiwango cha elimu ilivyo hivi sasa hasa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kufuatia kudorora kwa kiwango cha elimu kwa ujumla.
"Kwa mujibu wa takwimu kimazingira inaonyesha kuwa Chalinze ndani ya kipindi kati ya 2015 na 2020 wanafunzi wengi wamekua hawafanyi vizuri katika elimu ya msingi na sekondari ambapo wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali ndani na nje ya familia zao ambazo endapo tukiunganisha nguvu zetu kwa pamoja nina imani kubwa vijana wetu watashika madaraja ya juu katika kiwango cha elimu"alisema Alhaj Sharif.
Alisema kuwa wazazi na viongozi wote kwa pamoja wanajukumu la kutathmini juu ya mfumo mzima wa elimu namna ya ufundishaji kitafuta mbinu za kumwezesha mwanafunzi kuweza kuelewa masomo na kuwa na ari ya kusoma sambamba na wazazi kuwafuatilia watoto wao waendapo na kurudi kutoka shuleni.
"Hivi Sasa idadi ya vijana wa Chalinze wanaokwenda katika shule za vipaji ni wa chache hii ni tathmini ya mwaka 2016 na 2021 hivyo aliwaambia wanaJukwaa pamoja na wadau waliojitokeza kuhudhuria Kongamano Hilo la elimu kuwa wanapaswa kuto kata tamaa kutokana na changamoto mbalimbali walizozipitia" na zilizo jitokeza kala ya kufanyika kwa Kongamano hilo.
"Kupitia jukwaa hili la Wadau wa Elimu Chalinze litaweza kuatua mambo mengi kielimu sababu elimu ndiyo kila kitu katika maisha " alisema Shariff.
"Tupo hapa kujadili mustakabali wa elimu na mimi binafsi nawaaahidi kwamba nitakuwa bega kwa bega na nyinyi muda wowote na salaamu za jukwaa hili nitazioeleka panapostahili ikiwemo kuzungumza moja kwa moja na Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa kuna jukwaa ambalo linaundwa n watu makini wenye uchungu na Chalinze" alisema Mwenyekiti huyo.
"Suala la elimu liko ndani ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) nasisitiza Halmashauri ya Chalinze kwa pamoja na jukwaa waweke mikakati madhubuti itakayopandisha kiwango cha elimu ikiwemo kutoa hamasa kwa waalimu kuwekewa mazingira rafiki ya kufundisha"
Afisa Mipango Halmashauri ya Chalinze Shaban Milawoalisema kuwa wataanzisha utaratibu kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi mashuleni ikiwa ni katika kupambana na tabia ya utoro pia wataje ga nyumba za waalimu ikiwa ni katika kutoa hamasa ya kufundisha.
Jukwaa hilo la Wadau wa Elimu Chalinze liliasisiwa na watu wa kada mbalimbali miaka saba iliyopita pia limehudhuriwa na watu mbalimbali ikwemo, waalimu , vijana na baadhi ya Madiwani wa Jimbo hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...