Na Mwandishi wetu- MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) imesaini mkataba wa ushirikiano na Chama cha Madaktari China (CMA) pamoja na hospitali ya Tian Tan kwa lengo la kuboresha huduma za kibingwa hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface  wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba huo iliyofanyika kwa njia ya mtandao leo Jijini Dar es Salaam.

 “ Mkataba huu wa Ushirikiano unamanufaa makubwa upande wa gharama za vifaa tiba, kwani China ina viwanda vingi hivyo itasaidia MOI kupata vifaa tiba kwa bei nafuu  na kupelekea  gharama za matibabu  kushuka, ” Alisisitiza Dkt. Boniface

Akifafanua Dkt. Boniface amesema kuwa faida nyingine za mkataba huo ni kuimarisha ushirikiano baina ya MOI na CMA kwa kuwezesha wataalamu kutoka China kuja kutoa huduma nchini Tanzania na Wataalam wa Tanzania watapata fursa ya kwenda kujifunza nchini China.

Hafla ya utiaji saini imefanyika kwa njia ya mtandao na kuhudhuriwa moja kwa moja na  Balozi wa Tanzania nchini China Mh. Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface pamoja na wajumbe wa menejimenti ya MOI.

Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Balozi  Mbelwa Kairuki amesema hatua ya Taasisi ya  MOI kuingia mkataba na Chama cha Madaktari China (CMA) pamoja na hospitali ya Tian Tan italeta mapinduzi makubwa kwenye utoaji wa huduma za kibingwa za mifupa, ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu hapa nchini Tanzania.

Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) imesaini mkataba wa ushirikiano na Chama cha Madaktari China (CMA) pamoja na hospitali ya Tian Tan kwa lengo la kuboresha huduma za kibingwa hapa nchini ikiwa ni moja ya hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia MOI.

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface akiwasilisha mada wakati wa hafla ya utiaji saini kati ya MOI na chama cha Madaktari China (CMA).

. Balozi wa Tanzania nchini China Balozi Mbelwa Kairuki akiwa pamoja na viongozi wa Chama cha madaktari China (CMA) leo wakati wa utiaji saini kati ya MOI na chama hicho.(Picha zote na MOI)

Wajumbe wa Menejimenti ya MOI wakishuhudia hafla ya utiaji saini baina ya MOI na Chama cha Madaktari China (CMA) ili kuboresha huduma za kibingwa za Mifupa , Ubongo, Mgongo na Mishipa ya fahamu hapa nchini.

 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...