Na Khadija Kalili, Pwani
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge ameamuru kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa  Mtendaji wa Kata ya Mtambani  Wilayani Kibaha kwa kushindwa kudhibiti wakulima wa mbogamboga kwenye kitongoji cha Kwa Dosa ambao wanavuta maji kutoka chanzo cha mto Ruvu.

RC Kunenge  amezuia matumizi ya umwagiliaji na unyweshaji wa mifugo kwa watu wanaotumia vyanzo vya mito ili kukabiliana na upungufu wa maji kwenye mito ndani ya mkoa huo.
Alhaji  Kunenge ameyasema hayo leo alipotembelea kuangalia shughuli zinazofanywa kwenye vyanzo vya maji vya mto Ruvu eneo la Dosa na Kidogozero ambapo kuna baadhi ya watu wanajishughulisha na kilimo na unyweshaji mifugo kunakosababisha uhaba mkubwa wa maji kwenye Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam

Awali  Afisa wa Bonde la mto wami Ruvu  Halima Faraji amesema wamefanya hivi karibuni opereshen Kwenye maeneo hayo na kubaini wapo watumiaji wengi wa maji  wasio rasmi pamoja na mifugo

Pia amesema watumiaji maji 300 ndio wenye vibali wanaotambulika pekee.
Afisa huyo ameongeza kuwa, kwa data za novemba 15 walipofanya ukaguzi walikuta  maji Lita 4100 yalikuwa yanapita mtano humo kwa sekunde  na Sasa yameongezeka kwa sababu  data za Jana novemba 18  wamekuta Lita 6430 ndio zinapita kwa sekunde hivyo Kuna ongezekoa linaonekana maji yanaongezeka

RC  Kunenge ametoa agizo hilo leo alipotembelea bonde la mto Ruvu  akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na ya Wilaya za Kibaha,Kisarawe, na Bagamoyo .
 "Kuanzia leo Novemba 19 hakuna ruhusa mtu yeyote kufanya shughuli za umwagiliaji,kilimo wala kunyweshewa mifugo hadi hapo serikali itakapotoa maelekezo mengine.
"Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa na Wilaya tatu za Kibaha, Bagamoyo na Kisarawe tumekuja kufanya ukaguzi wa eneo la bonde la mto Ruvu ukiwa niutekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan alivyoelekeza shughuli za kilimo na umwagiliaji kwenye maeneo ya vyanzo vya maji visimame kwanza kwani  wakati huu kuna uhaba wa maji " alisema  RC Kunenge.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...