Na WAMJW-DOM
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt .Dorothy
Gwajima amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la
Maendeleo la USWISI Bi. Patricia Danzi aliyeambatana na ujumbe kutoka
Shirika hilo.
Katika kikao hicho kwa pamoja wamekubaliana
kuendelea kuimarisha ushirikiano katika kuketa Maendeleo nchini hususan
katika eneo la huduma za afya kwa Watanzania.
Dkt. Gwajima
amesema, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya
Afya inaendelea kuboresha huduma za afya, na sasa ipo mbioni kupitisha
sheria ya Bima ya Afya kwa wote itayomruhusu kila mwananchi kuwa na Bima
ili kupata huduma za matibabu.
Aliendelea kusema kuwa, kama
nchi inaendelea kuimarisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria kwa
kupitia afua mbalimbali ikiwemo utoaji elimu kwa wananchi juu ya njia
bora za kujikinga dhidi ya Malaria na ujenzi wa kuwanda cha viuadudu
kilichopo Mkoa wa Pwani.
Aidha, Dkt. Gwajima amesema kuwa,
Tanzania inaendelea na mapambano dhidi ya UVIKO-19 kupitia afua ya Elimu
kwa wananchi juu ya njia bora za kujikinga dhidi ya UVIKO-19 na utoaji
wa Chanjo ya UVIKO-19, huku akieleza tayari Tanzania imepokea Chanjo
tofauti ikiwemo Jenseen, Sinopharm na Pfizer.
Kwa upande wake
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la USWISI Bi. Patricia Danzi
amesema Serikali ya Uswisi imekuwa mdau mzuri wa mapambano dhidi ya
UVIKO-19 kwa kuchangia zaidi ya Dozi 4,000,000 kupitia mpango wa COVAX
Facility ambapo Tanzania ni moja ya wanufaika wa mpango huo.
Viongozi
hao wamekutana leo, katika ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma na
kikao hicho kimehudhuriwa na baadhi ya Maafisa kutoka Wizara ya Afya na
Shirikishi la Maendeleo la Uswisi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...