Watanzania kutoka sehemu mbalimbali za nchi wakiwamo waliohudhuria tamasha la muziki wamemshuhudia Abbas Mohamed Mwinyimkuu wa Kawe, jijini Dar es Salaam, akijishindia zawadi ya bodaboda mpya iliyochezeshwa katika Uwanja wa Tanganyika Packers, iliyoandaliwa maalum kwa ajili ya wadau na mashabiki wa muziki kwa kupitia tamasha la Komaa lililoendeshwa chini ya udhamini mnono wa Kampuni ya Biko, waendeshaji wa bahati nasibu inayoongoza kutoa washindi wengi nchini Tanzania.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Mwinyimkuu shabiki na mwanachama maarufu wa klabu ya Simba, alisema alijaribu kucheza biko kwa mara ya kwanza uwanjani hapo Jumamosi ya Desemba 4 asubuhi, huku jioni yake akipigiwa simu ya ushindi.

Mbali na ushindi huo wa droo ya bodaboda kwa Mwinyimkuu, biko inaendelea kutoa zawadi nono kuanzia sh 2500 hadi Sh Milioni 5 papo hapo, bila kusahau droo kubwa ya zaidi ya Sh Milioni 40 kila Jumapili ambapo kwa sasa imerahisishwa ambapo Watanzania wanaweza kucheza live kwa kuingia mtandaoni www.biko.co.tz pamoja na wanaotumia simu za kawaida kwa kuweka namba ya Kampuni ya 505050 na kumbukumbu 2456.


Biko mchezo unaochezwa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi unachezwa kwa kufanya miamala kuanzia sh 1000 na kuendelea kwa kuchungulia nafasi, mchezaji anapaswa kuweka namba yake ya simu na fedha kuanzia sh 1000 na kuendelea na kubonyeza kitufe cha Cheza Sasa kwa ajili ya kuwahi nafasi za ushindi, huku kila mtu aikiona live jinsi mduara unavyozunguuka na washindi wanavyopatikana katika bahati nasibu hiyo ya aina yake.

Mshindi wa bodaboda ya Biko Abbas Mwinyimkuu ambaye pia ni mwanachama wa klabu ya Simba na Mwenyekiti wa Tawi la Simba Kawe akiwa juu ya pikipiki aliyoshinda kutoka kwenye bahati nasibu ya Biko Jumamosi iliyopita katika Viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar es Salaam, katika Tamasha la Komaa Concert lililoandaliwa na EFM Radio, huku Biko wakiwa sehemu ya wadhamini wa tamasha hilo. Picha na Mpigapicha wetu.



Mshindi wa bodaboda ya Biko Abbas Mwinyimkuu ambaye pia ni mwanachama wa klabu ya Simba na Mwenyekiti wa Tawi la Simba Kawe, akipokea karatasi muhimu za umiliki wa hicho cha usafiri kutoka kwa waendeshaji wa bahati nasibu ya Biko ikiwa ni zawadi maalum iliyoandaliwa katika Tamasha la muziki la Komaa Concert lililofanyika viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar es Salaam, chini ya EFM Radio kwa udhamini mnono wa Biko. Anayekabidhi nyaraka hizo ni Meneja Masoko wa Biko Goodhope Heaven na kushuhudiwa na mtangazaji wa EFM, Jackilne Charles kushoto. Picha na Mpigapicha Wetu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...