Na. John Mapepele

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo amekitaka chama  cha kuogelea nchini kushirikisha mikoa yote nchini  ili kupata waogeleaji wenye vipaji watakaoiwakilisha vema Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa.

Mhe. Gekul ameyasema haya leo Disemba  4, 2021jijini Dar es Salaam allipoambatana  na Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa( BMT) Neema Msitha kuikabidhi bendera na kuiaga timu ya Tanzania inayokwenda kushiriki  mashindano ya Afrika ya kuogelea nchini Uganda.

Aidha, amewapongeza wazazi kwa kuwaruhusu watoto kushiriki katika  mchezo huu.

"Niwapongeze wazazi kwa mwamko mkubwa wa kuwarushusu watoto kujiunga kwenye mchezo huu, hii itasaidia kupata vipawa na vipaji vingi " amefafanua Mhe. Gekul

Amesema Serikali imeshaandaa Mpango Mkakati wa miaka kumi wa kuinua na kuendeleza michezo ili kuinua michezo.

Naye Msitha amemweleza Mhe. Naibu Waziri kuwa chama cha  mchezo wa kuogelea ni miongoni mwa vyama vya michezo  inayofanya kazi nzuri ya kuinua mchezo huu hapa nchini.

Kiongozi wa timu hiyo Inviolata Itatilo amesema nchi zaidi ya kumi za Afrika  zinashiriki mashindano haya nchini Uganda.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...