Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Kagera limefanikiwa kumuokoa mtoto mchanga aliyekuwa ametupwa chooni jana tarehe 01 Desemba, 2021 huko wilayani Karagwe kata ya Bugene katika Mtaa wa Lukajage.

Mtoto huyo wa Kiume anayesadikiwa kuwa na umri wa Siku Mbili alitupwa katika choo hicho na mtu ambaye hakufahamika mara moja na sasa yupo katika Hospitali ya Kayanga Wilayani Karagwe akiendelea na matibabu. Jeshi la Polisi Mkoani Kagera linaendelea na uchunguzi ili kumbaini mama wa mtoto huyo.

Kaimu Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji (M) Kagera Mkaguzi Thomas Majuto amesema, walipata taarifa kwa njia ya simu na kuwahi kufika eneo la tukio kisha kufanikiwa kumuokoa Mtoto huyo. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)


Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji S/Sgt Karata Ramadhani Karata akimpatia huduma ya kwanza mtoto mchanga aliyemuokoa kutoka katika shimo la choo alikokuwa ametupwa huko Mkoani Kagera, Wilaya ya Karagwe Kata ya Bugene tarehe 01 Desemba, 2021

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...