NA VICTOR MAKINDA: MVOMERO

 MKUU wa Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro,  Halima Okash, ameziomba Asasi za Kiraia (AZAKI) zinazofanya shughuli zake wilayani hapa, kusaidiana na viongozi wa ngazi  viongozi wa ngazi mbali mbali  pamoja na kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya kutafuta suluhu ya kudumu ya migogoro baina ya wakulima na wafugaji.

Okash alitoa ombi hilo jana Novemba 30 wakati wa mkutano baina yake na  Asasi za Kiraia uliolenga kujadili na kupendekeza mbinu za usuhulishi wa kudumu wa migogoro ya wakulima na wafugaji wilayani hapa.

“ Pamoja na jitihada kubwa ambazo serikali inafanya kuimaliza migogoro kati ya wakulima na wafugaji wilayani Mvomero, lakini bado kuna viashiria vya uwepo wa migogoro baina ya makundi hayo. Nimewaita ndugu zangu wa Asasi za Kiraia mnaofanya kazi zenu wilayani hapa, ili kwa pamoja tujadili na kupendekeza mbinu muafaka ambazo zitasaidia kumaliza kabisa migogoro hiyo. Alisema Okash.

Katika hatua nyingine Okash alizitaka Asasi za Kiraia zinazofanya kazi wilayani hapa kujielekeza katika kutekeleza miradi ambayo ina matokea chanya ya moja kwa moja kwa jamii ili kusukumu kwa haraka gurudumu la Maendeleo ya wilaya ya Mvomero na Tanzania kwa ujumla.








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...