Na Pamela Mollel,Arusha

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Tulia Ackson amekipongeza chuo Cha uhasibu Arusha kwa kutoa aina ya mitaala ambayo inazingatia umahiri kwa wahitimu na uhalisia wa jamii.

Mhe Ackson ameyasema hayo wakati alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 23 ya wahitimu wa chuo Cha uhasibu Arusha .

Amesema kuwa anakipongeza chuo hicho kwani kinatoa aina ya mitaala ambayo inazingatia umahiri na utaalamu wa kuwafanya wahitimu kujiajiri lakini pia kuhudumia jamii kupitia taaluma walizozipata.

Kwa upande wake Mkuu wa chuo Cha uhasibu Arusha profesa Eliamani Sedoyeka amesema kuwa matarajio ya chuo Ni kuwa wanatarajia wahitimu hao kutumia maarifa na ujuzi walioupata chuoni hapo kuhudumia jamii na taifa kwa ujumla

Alisema kuwa mpaka sasa Chuo hicho kinatoa mafunzo ya kuanzia ngazi ya Astashahada,Stashahada,Shahada na Shahada ya Uzamili

"Mpaka sasa chuo kinatoa takribani kozi 17 kwa ngazi ya cheti /Astashahada,kozi kumi na saba ngazi ya Stashahada,kozi kumi na nane ngazi ya Shahada na kozi kumi na mbili za Shahada ya Uzamili"alisema Sedoyeka

Aliongeza kuwa chuo hicho kimejipanga kusaidia serikali kukabiliana na changamoto ya ajira kwa kuandaa mitaala inayoendana na soko la ajira Kitaifa na Kimataifa katika maeneo ya Uhasibu,Tehama,Fedha,Uchumi,Kodi,Utawala,Bima,Ukutubi,Utalii,Ugavi na Ununuzi

"Mitaala yetu inawaandaa wanafunzi kuajiriwa lakini pia wanaandaliwa kwa namna ambayo wanaweza kujiajiri wenyewe na kutimiza malengo binafsi na yakitaifa pia"Alisema Sedoyeka

Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi ya chuo Cha uhasibu Arusha dkt Mwamini Tulli amesema kuwa chuo kinaendelea kutoa mafunzo yenye mitaala ya kuwezesha wahitimu wajiajiri hivyo kuweza kupambana na soko la Sasa .

Alimpongeza Mkuu wa Chuo Cha Uhasibu Arusha, Prof. Eliamani Sedoyeka, Menejimenti ya Chuo na Watumishi wote wa Chuo kwa kazi nzuri waliyofanya ambayo imefanya Chuo kufikia katika hatua kubwa ya maendeleo

Aidha alihaidi kushirikiana kikamilifu na kufanya kazi na Uongozi wa Chuo ili kuhakikisha kwamba mikakati ambayo Chuo kimejiwekea katika utekelezaji wa majukumu yake ya kutoa mafunzo, kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu inatekelezwa ili kulinda hadhi ya Chuo ambayo kimejijengea hapa nchini

Kushoto ni Mkuu wa Chuo cha uhasibu Arusha Profesa Eliamani  Sedoyeka akiteta jambo na Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Tulia Ackson katika mahafali ya 23 ya wahitimu wa chuo cha uhasibu Arusha
Mwanafunzi bora Anastazia Shayo akifurahia zawadi alizozipata katika mahafali hayo
Katibu Mkuu wa umoja wa vijana wa Chama Cha mapinduzi kenani kihongosi ni mmoja wa wahitimu waliohitimu katika mahafali hayo ya 23


Wahitimu wa chuo cha uhasibu Arusha wakiwa katika mahafali ya 23 jijini Arusha
Mwakilishi wa wahitimu Michael Munichi aipongeza chuo hicho pamoja na wahitimu kwa kufikia hatua hiyo
Kushoto ni Mkuu wa Chuo cha uhasibu Arusha Profesa Eliamani  Sedoyeka akiteta jambo na Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Tulia Ackson katika mahafali ya 23 ya wahitimu wa chuo cha uhasibu Arusha
Mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha Eliamani Sedoyeka  akizungumza na wahitimu  katika mahafali ya 23 jijini Arusha
Spika wa Bunge la Tanzania Tulia Ackson akifafanua jambo katika mahafali hayo yaliyofanyika leo jijini Arusha
Mwenyekiti wa Baraza la uongozi wa chuo cha uhasibu Arusha Dkt,Mwamini Tulli akizungumza katika mahafali hayo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...