Serikali imeokoa takribani Shilingi Bilion 4 baada ya kuamua kutekelezwa mradi wa Maji Kirando kwa Mfumo wa Force Akaunti kwa kutumia Taasisi zilizochini ya Wizara ya Maji ambazo ni Mamalaka ya Maji Sumbawanga na Wakala wa Maji Vijijini RUWASA.
Mradi huo ulitakiwa kutekelezwa kwa Bilion 7.7 na sasa utatekelezwa mpaka mwisho kwa Bilion 3.1
Mradi wa Maji Kirando ambao unatumia chanzo Cha Ziwa Tanganyika umekamilika kwa Wastani wa Asilimia 95 na umeanza kuwanufaisha Wananchi wa Vijiji 7 vya Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa.Kabla ya mradi kuanza kutoa huduma ya Maji, Wananchi wa Kirando walikuwa wanatumia Maji ambayo si safi wala salama katika madimbwi ya Maji.
Mradi huo utawanufaisha Wakazi 74,341.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...