Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV
WEKUNDU wa Msimbazi Simba SC wamefuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF Confederation Cup) msimu wa 2021-2022 baada ya ushindi wa jumla wa mabao 4-2 dhidi ya Red Arrows ya Zambia katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la Mashujaa mjini Lusaka nchini Zambia.
Simba SC licha ya kucheza chini ya kiwango katika mchezo huo ilipokea kichapo cha bao 2-1 kutoka kwa wenyeji Red Arrows katika mchezo huo wa mkondo wa pili. Simba SC walipata ushindi wa bao 3-0 katika mchezo wa mkondo wa kwanza wiki moja iliyopita nyumbani Banjamin Mkapa, Dar es Salaam, Tanzania.
Katika mchezo huo, wa pili Red Arrows walipata mabao yao mawili kupitia kwa Wachezaji Ricky Banda na Sadam Phiri wakati bao la Hassan Dilunga likiwakatisha tamaa kabisa Red Arrows katika mchezo huo.
Simba SC wanafuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika badala ya kushindwa kufuzu hatua hiyo kwenye Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League) siku chache baada ya kutupwa nje na Klabu ya Jwaneng Galaxy FC ya Botswana wakati nyumbani Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...