Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya Usafiri wa Anga Duniani, Mamlaka imeendesha mafunzo Kwa watoto wa watumishi wa TCAA kuhusu Usafiri wa Anga na  kufanya ziara katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ili kupata elimu kuhusu kazi zinazofanywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa semina hiyo Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti Uchumi Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Daniel Malanga  amesema Mamlaka hiyo imeamua kuandaa semina ili kuweza kutoa elimu kwa watoto hao ili waweze kujua kazi zinazofanywa na Mamlaka hiyo kwa nadharia pamoja na vitendo.

Pia amesema watoto ni taifa la kesho hivyo wanapaswa kuandaliwa vyema ili kuweza kufikia malengo pamoja na ndoto zao hivyo wanapaswa kusimamiwa kwa kupewa elimu iliyobora na yenye tija kwa maisha yake ya baadae.

Amesema elimu watakayoipata kwenye semina hiyo isiishie hapo bali iwe chachu kwao na wakawe mabalozi wazuri wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kwa watoto wenzao wa mtaani pamoja na shuleni.
Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti Uchumi Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Daniel Malanga  akizungumza na wanafunzi wa watoto wa watumishi wa TCAA waliofika kwenye semina ili kupata elimu kuhusu kazi zinazofanywa na Mamlaka hiyo
Rais wa Chama cha Waongozaji ndege Tanzania (TATCA), Shukuru Nziku akitoa semina kwa watoto wa wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) waliofika kwenye Mamlaka hiyo ili kupata elimu ya kazi zizofanywa na mamlaka hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Watoto wakiwa kwenye chumba cha kuongezea ndege kilichopo katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Watoto wakiwa kwenye picha ya pamoja


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...