Na. Eleuteri Mangi,GCU, WUSM


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa ushirikiano kwa Serikali ya Jamhuri ya Zimbabwe kutambua maeneo yote ambayo yalitumiwa na wapigania uhuru wa Zimbabwe kwa lengo la kutunza historia ya nchi hizo mbili kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Waziri Bashungwa amesema hayo leo Desemba 17, 2021 wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Habari na Utangazaji wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Monica Mtsvangwa jijini Dodoma.

Ziara ya Mhe. Mutsvangwa nchini inalengo la kutambua, kukusanya na kuhifadhi taarifa na kumbukumbu za harakati za ukombozi wa Zimbabwe zilizopo hapa nchi katika mfumo wa kidigitali.

Kwa upande wake Waziri wa Habari na Utangazaji wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Monica Mtsvangwa ameishukuru Tanzania kwa kutenga na kuanzisha maeneo ya kambi za kuwaandaa wapigania uhuru wa nchi yao na wanaamini watapata taarifa ambazo zitawasidia kutengeneza makala maalumu ya historia ya ukombozi wa taifa lao yatakayotumika kutoa elimu kwa wananchi wa Zimbabwe.

Maeneo ambayo msafara wa Waziri Mhe. Mutsvangwa watayatembelea ni Nachingwea mkoani Lindi, Mgagao mkoani Iringa, Kongwa mkoani Dodoma, Chunya mkoani Mbeya na Bagamoyo mkoani Pwani.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa katikati akizungumza na ujumbe kutoka Zimbabwe uliofika hapa nchini ukiongozwa na Waziri wa Habari na Utangazaji wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Monica Mtsvangwa kwa ajili ya kuzalisha makala maalumu ya historia ya ukombozi wa taifa lao yatakayotumika kutoa elimu kwa wananchi wa Zimbabwe.


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa akimsikiliza Waziri wa Habari na Utangazaji wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Monica Mtsvangwa wakati wa mazungumzo baina yao kuhusu uzalishaji wa makala maalumu ya historia ya ukombozi wa taifa la Zimbabwe yatakayotumika kutoa elimu kwa wananchi wa Zimbabwe.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari na Utangazaji wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Monica Mtsvangwa mara baada ya mazungumzo yao kuhusu kuzalisha makala maalumu ya historia ya ukombozi wa taifa la Zimbabwe yatakayotumika kutoa elimu kwa wananchi wa Zimbabwe.



Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa akiagana na Waziri wa Habari na Utangazaji wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Monica Mtsvangwa mara baada ya mazungumzo yao kuhusu kuzalisha makala maalumu ya historia ya ukombozi wa taifa la Zimbabwe yatakayotumika kutoa elimu kwa wananchi wa Zimbabwe.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...