Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi akisaini mkataba wa makubaliano ya kimkakati na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kukuza ukusanyaji wa mapato sekta ya utalii.


Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki yaN NMB, Filbert Mponzi akizungumza na wageni waalikwa kabla ya kusaini mkataba wa makubaliano ya kimkakati na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kukuza ukusanyaji wa mapato sekta ya utalii.



……………………………………..

Benki ya NMB imesaini makubaliano ya kimkakati na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kushirikiana katika kuimarisha na kukuza ukusanyaji wa mapato kwenye sekta ya utalii visiwani humo kupitia mifumo ya kidijitali.

Makubaliano hayo yamesainiwa leo na Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Fatma Mabrouk Khamis.

Kupitia ushirikiano huu, Benki ya NMB itachagiza shughuli za kitalii kupitia;

ambapo itawekeza kwenye mfumo wa kidigitali utakaotumika kufanya makusanyo ya Serikali katika vituo vyote vya utalii Zanzibar

Itasambaza mashine za malipo (POS) kwenye vituo vya makusanyo na vivutio vya utalii. Hii itawawezesha watalii kulipia ada na tozo zote kupitia kadi zao za Mastercard, Visa na UnionPay

Pia itatoa elimu na kuhamasisha watu kuzidi kutembelea vivutio vya kitalii vilivyopo visiwani humo kupitia matamasha na promosheni mbali mbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...