Charles James, Michuzi TV
NI TULIA Ackson! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia jina la Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson kupitishwa na Chama Cha Mapinduzi kugombea nafasi ya uSpika wa Bunge.

Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dodoma leo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Shaka Hamdu Shaka amesema kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama hicho kujadili na kuchambua orodha ya wagombea waliochukua fomu ya kuwania kiti hicho na hivyo kuteua Jina la Naibu Spika huyo.

Shaka amesema hatua inayofuata baada ya Kamati Kuu kufanya maamuzi hayo ni jina la Dkt. Tulia kwenda kupigiwa kura kwenye kikao cha Wabunge wa Chama hicho (Cocas).

Jina la Dkt Tulia limepitishwa baada ya mchujo uliofanyika ambapo wanachama 70 wa wa Chama hicho walichukua fomu ya kugombea nafasi hiyo baada ya aliyekua Spika, Job Ndugai kujiuzulu mapema mwezi huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...