Na John Walter-Hanang
KUTOKANA na uhaba wa maji unayoikumba shule ya sekondari Daniel Naud iliyopo kata ya Mogitu wilayani Hanang, Mbunge wa jimbo la hilo Mhandisi Samweli Hayyuma amesema Siku chache zijazo RUWASA watasaini mkataba na waziri wizara ya Maji ili kuanza utekelezaji wa mradi utakaohudumia kata za Gehandu na Mogitu.

Akizungumza mbele ya kamati ya siasa ya wilaya ya Hanang mheshimiwa Hayyuma amesema licha ya kuwepo kwa changamoto ya maji katika shule hiyo ameitaka kamati ya shule hiyo kumalizia kuweka vigae katika sehemu iliyobaki ili shule hiyo iwe ya kisasa na inayokwenda na wakati.

Akijibu ombi la Mbunge mkuu wa wilaya ya Hanang Janeth Mayanja amesema kutokana na vifaa vya ujenzi vilivyobaki muda sio mrefu watabadili na kuchukua vigae ili wamalizie sehemu iliyobaki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...