Na Mwamvua Mwinyi Pwani,
Mkuu
wa mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amewataka wananchi wa Mafia kuwa na
tabia ya kusaidiana kunapotokea changamoto athari mbambali ili kupunguza
madhara yanayoweza kujitokeza.
Kunenge
aliyasema hayo kwenye ziara ya kukagua athari za zilizosababishwa na
mvua kubwa pamoja na upepo mkali ambapo ambapo maafa yaliyojitokeza ni
pamoja na kukatika kwa Tishari bandari ya kilindoni miti mikubwa
kuangukia makazi ya watu pamoja na kaya zaidi 46 kuathiriwa na mvua
hizo.
Alieleza,
mkoa wa Pwani umekumbwa na maafa ikiwemo Mafia, Kibiti, Mkuranga,
Rufiji,Chalinze nyuma 36 pamoja na madarasa mawili kuezuliwa mabati na
Upepo mkali kule shule ya Makombe,na Kisarawe nyumba 100.
"Mvua
kubwa zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta maafa
Mkoa hapa, tuendelee kusaidia pale inapotokea shida na Serikali
itaangalia namna ya kutia nguvu yake."alifafanua Kunenge.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mafia Martin Ntemo alieleza hatua walizochukua ni kufika eneo la tukio na kuunda timu ya kufanya tathmini ili kujua ukubwa wa maafa yaliyojitokeza.
Baadhi ya wananchi waliothirika na athari hiyo wameiomba Serikali iwasaidie hasa katika kuwapimia maeneo wanayoishi yasiyo rasmi ili waishi kwa usalama zaidi.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mafia Martin Ntemo alieleza hatua walizochukua ni kufika eneo la tukio na kuunda timu ya kufanya tathmini ili kujua ukubwa wa maafa yaliyojitokeza.
Baadhi ya wananchi waliothirika na athari hiyo wameiomba Serikali iwasaidie hasa katika kuwapimia maeneo wanayoishi yasiyo rasmi ili waishi kwa usalama zaidi.
"Tunashukuru
viongozi kutukimbilia kuja kutupa pole,kitongoji hiki
hakijapimwa,tunaishi kiholela, Serikali ifanye mkakati wa kutupimia ili
tuishi kama wengine kwenye maeneo rasmi "walisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...