SERIKALI imekiasa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji NIT kuendelea kuzalisha wataalamu wengi zaidi katika sekta ya usafirishaji na Uchukuzi watakaosaidia kuendesha miradi inayofanywa na serikali ili kukuza uchumi wa nchi.

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atupele Mwakibete amesema hayo leo Januari 26,2022 wakati wa ziara yake chuoni hapo  na kujifunza mambo mbalimbali.

Amesema,  chuo cha Usafirishaji ni muhimu kwa uchumi wa Taifa ambo unategemea usafirishaji na Uchukuzi, hivyo ni ndoto kubwa kwa wizara yake kuona wataalamu wa sekta hiyo wanatoka hapa nchini.

"Nikiwa chuoni hapa nimejionea vitu vingi ikiwemo mifumo itakayotumika kiwafundishia  marubani,  ukaguzi wa gari shughuli nyinginezo jambo ambalo ni hatua kubwa kwa nchi" amesema Mwakibete.

Aidha amewashauri wasafirishaji na wamiliki wa vyombo vya moto kunitumia Chuo hicho kwa kujifunza ilk kuweza kuepuka ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikua wananchi wengi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo hicho Profesa Zakaria Mganilwa amesema, chuo kitaendelea Chuo wataalamu katika nyanja zote za sekta hiyo kwani jukumu lao kubwa walilopewa na serikali kufundisha wataalamu watakaosaidia kuendesha miradi ya inayofanywa na serikali.

 Amesema, Serikali imefufua Shirika la ndege ATCL, na inajenga reli ya kisasa hivyo kwa kuangalia hayo sasa wako katika hatua ya mwisho ya kukamilisha mchakato wa kufundisha kozi ya urubani wa ndege kwa garama nafuu ya shilling milioni 70.

Amesema kuwa kati ya fedha hizo Sh21 milioni ni gharama za kozi hiyo ngazi ya awali ambayo itamuwezesha mwanafunzi kusoma masomo ya awali na kuruka angani saa 50.

Amesema ingawa bado hawajapata ndege za mafunzo ila wanatarajia muda siyo mrefu watapata ndege hizo ili waweze kuanza kuzalisha wataalamu kwa mtandao wote wa sekta ya anga.

"Chuo hiki kumekuwa kikitoa mchango mkubwa wa kukuza uchumi nchini kwa kuzalisha rasilimali watu sahihi kwa ajili ya sekta nzima ya uzalishaji na Uchukuzi.
Ameongeza kuwa, chuo pia kimepata eneo la ekari 1000 jijini Dodoma karibu na uwanja wa ndege wa Msalato ambalo watalitumia  kwa ajili ya kutengeneza mabehewa.

"Eneo letu hapa ni dogo ndio maana tumetafuta eneo hili kama tulivyotafuta eneo mkoani Mtwara lengo kuu likiwa kutanua wigo wa huduma zetu",amesema Profesa Mganilwa.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atupele Mwakibete akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kumaliza kutembelea Kituo cha Kupima Magari kilichopo katika Chuo cha Taifa {NIT} wakati wa ziara yake  katika chuo hicho, jijini Dar es Salaam leo Januari 26, 2022.
jijini Dar es Salaam leo Januari 26, 2022.








Matukio mbalimbali wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atupele Mwakibete katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji {NIT}jijini Dar es Salaam leo Januari 26, 2022.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...