Na Humphrey Shao, Michuzi Tv

Waziri wa Uwekezaji Viwanda na Biashara, Dkt.Ashatu Kijaji ametoa siku tatu kwa tume ya ushindani nchini (FCC), kutoa majibu ya kupanda kwa bei ya vinywaji na kupotea sokoni. Pia ametoa siku saba kwa FCC, kutoa majibu ya kupanda kwa bei ya vifaa vya ujenzi nchini ikiwemo nondo na saruji.


Dk.Kijaji Amesema hayo Leo wakati alipofanya ziara yake ya kwanza tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo katika ofisi za FCC Mkoani Dar es Salaam.

Dk. Kijaji Amesema Mje na majibu ya haraka katika ya kupanda kwa bidhaa hizo katika kipindi hiki, hali inayopelekea changamoto kubwa kwa wananchi.

Amesema kumekuwepo na hali ya upandishaji wa bidhaa mara kwa mara bila ya kuwepo sababu za msingi, huku FCC wakiwa kimya.

" Hii sio sahihi, tupo kwaajili ya kulinda walaji, sasa kama hali inaenda hivi na nyie mnakaa kimya, sidhani kama mnatekeleza wajibu wenu ipasavyo.

Aliwataka kufanya chunguzi makini zinazotoa majibu haraka na sahihi kabla ya wananchi kupata athari.

Aliwataka FCC kujiuliza je ni sahihi tatizo litokee kwa jamii ndio watoe majibu au wanatakiwa kutambua changamoto mapema kupitia chunguzi zenu na kueleza jamii njia sahihi ya kuepuka changamoto hizo

Waziri Kijaji aliitaka FCC kutokaa kimya katika changamoto mbalimbali zinazojitokeza hasa za upandaji wa bei ya bidhaa ikiwemo za ujenzi na vinywaji.

" Ni vyema mkafanya chunguzi zenu vizuri kwa kina na haraka, ilikubaini sababu yakubadilika kwa bei za bidhaa mbalimbali sokoni kwa vipindi flani,"

Mnatakiwa kutembelea katika viwanda mbalimbali vya uzalishaji, ilikujionea hali halisi ya uzalishaji, kulinganisha na bei ya bidhaa zinavyouzwa sokoni.

" Mkifanya hivyo mtaweza kubaini changamoto ya mabadiliko ya bei ilikuruhusu majadiliano na wazalishaji juu ya kuweka bei rafiki inayoendana na hali halisi ya maisha ya wananchi.

Alisema FCC ni moyo wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara, hivyo ndiyo inayoweza kuamua kubadilisha kuleta maendeleo makubwa.

" Tumeaminiwa na kupewa majukumu haya mazito, hivyo nimeamua tusongembele kama kuna mtu ambaye hataki hilo na kutaka turudi nyuma sehemu hii sio yake atupishe," alisisitiza

Waziri Kijaji alisema hatovumilia uzembe wowote na uvivu na kusema kuwa anatamani kuona mwendo wa mchaka mchaka ili kutimiza malengo.

Pia aliwataka kufanya uchunguzi na kuhamasisha uzalishaji wa bidhaa bora nchini zinazo endana na uhitaji wa soko huria la sasa.

" Nivyema mkajitathimini ili kuboresha mipango yenu ili kufikia malengo na matarajio ya wananchi. Mkumbuke mmeshikiria uhai wa wananchi kupitia kuwalinda walaji kwa ukaguzi wa bidhaa feki hivyo endelezeni kwa juhudi adhima hiyo," alisisitiza.


Waziri Kijaji aliwaahidi FCC kuongezewa wafanyakazi kwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ameahidi kuajiri zaidi ya wafanyakazi 15000.

Pia Waziri huyo alimpongeza Rais Samia kwa kumwamini na kumteua kuwa Waziri na kusema atahakikisha anatimiza malengo ya kuaminiwa kwake kushirikiana na FCC.

Kwa upande wake Dk. Godwin Otieno mwakilishi wa Mwenyekiti wa bodi hiyo, alimshukuru Waziri Kijaji kwa kutambau umuhimu wa FCC nakufanya ziara yake ya kwanza ofisini hapo toka ateuliwe na Rais Samia.

" Tunakuahidi ushirikiano wakutosha katika majukumu yako haya.Pia tunatambua kazi kubwa uliyo kutokana na ukubwa wa wizara hii na umuhimu wake kwa jamii hivyo tutakuwa bega kwa bega na wewe," alisema.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa FCC, William Erio alimshukuru Waziri Kijaji na kuahidi kutekeleza maagizo yake aliyoyatoa.

Akieleza kazi yao ambayo wameifanya kwa miezi sita Juni hadi disemba mwaka Jana alisema wamefanya ukaguzi wa makontena 2831 katika bandari ya Dar ea salaam.

Alisema makontena 258 yalikamatwa yakiwa na bidhaa bandia ikiwemo vifaa vya magari na stationari.

Mkurugenzi mkuu alisema katika kwaka huu wamejidhatiti kutekelza majukumu yao ikiwemo, kulinda walaji, kufanya ukaguzi wa muungano wa makampuni.

" Wizara hii ni kiini cha ukuaji wa uchumi wa Taifa hivyo nafurahi na kumpongeza Rais Samia kwa kuniamini na kunipa jukumu hilo kubwa"

Waziri Mh.Dkt Kijaji alisema jukumu hilo analiweza hivyo atashirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo FCC ilikutimiza adhima ya Rais Samia kumteua katika Wizara hiyo.

"Naamini inawezekana kutekeleza jukumu hili muhimu, nimeamua tufanikiwe na asiyetaka hili sio sehemu yetu"

Akieleza sababu ya kufanya ziara yake ya kwanza FCC, alisema nikutokana na umuhimu mkubwa wa taasisi hiyo katika Wizara yake hiyo ya Uwekezaji, Viwanda, na Biashara

" Tume ya ushindani ni moyo wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara na mnaweza kuamua tusonge mbele au tusiende, ila nitahakikisha tuaenda"

Dkt.Ashantu Kijaji aliwapongeza tume hiyo kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya ya kuwalinda walaji nchini.

" Mnafanya kazi kubwa lakini niwatake muone namna ya kujiboresha ilikufikia malengo na matarajio ya wananchi"


Waziri wa Uwekezaji Viwanda na Biashara,Dk Ashatu Kijaji akizungumza na Waandishi wa habari pamoja na wafanyakazi wa FCC katika ofisi ndogo zilizopo Dar es Salaam.

 
 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...