Akizungumza baada ya kukagua Mradi huo, IGP Sirro, amesema kuwa Umaliziaji wa jengo hilo unatokana na fedha kiasi cha Bilioni 1.4 zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Wakati huo huo akiwa Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya IGP Sirro pia amekagua Mradi wa ujenzi wa jengo la ofisi ya kamanda wa Polisi ambapo ndani ya siku 100 tangu kutolewa kwa fedha kiasi cha bilioni 1.5 ujenzi huo umefikia hatua mbalimbali za kukamilika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...