Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Polisi kushirikiana na wananchi na viongozi mbalimbali katika kukabiliana na mauaji na watu kujiua.

Rais Samia ametoa agizo hilo wakati akihutubia kwenye Sherehe za Jubilee ya miaka 25 ya Utumishi wa Askofu Severine Niwemugizi zilizofanyika katika viwanja vya posta, wilaya ya Ngara mkoani Kagera.

Rais Samia amesisitiza kwamba harakati hizo lazima ziwe shirikishi kwani viongozi wa mitaa na vijiji ndio wanaowafahamu watu wao ambao wamekuwa moja ya chanzo cha mauaji hayo.

Takwimu zinaonesha kwamba mwaka 2020, wilaya ya Ngara pekee kulikuwa na matukio 22 ya mauaji na mwaka 2021 kulikuwa na matukio 21 huku kukiwa na matukio matatu ya watu kujiua mwaka 2020 na mawili mwaka 2021.

Ripoti za uchunguzi huonyesha sababu za ongezeko la matukio ya mauaji na kujiua mara nyingi ni kutokana na wivu wa kimapenzi, kuwania mali, kulipiza visasi, imani za kishirikina, ugomvi wa kifamilia pamoja na msongo wa mawazo.

Rais Samia amesema ameshaliagiza Jeshi la Polisi kufanya utafiti wa kujua sababu za kuongezeka kwa matukio ya mauaji hayo ili kuweza kufanya mikakati ya kupambana na tatizo hilo.

ZuhuraYunus
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...