Shule ya Academic Achievement ya jijini Dar e salaam imeeendesha mashindano ya vipaji na sayansi kwa wanafunzi wa sekondari na shule za msingi

Akizungumza wakati wa maonyesho hayo Mkurugenzi wa  Tasisi ya shule za Academic Achievement school,  Abdullah Zakharia amesema lengo la kuendesha mashindano hayo nikujaribu kuvumbua vipaji kwa wanafunzi ambao wengine katika shule zao hawaja pata hizo fursa

Aidha amesisitiza kuwa wamezialika zaidi ya shule kumi za jijini Dar es salaa kwa ajili ya maonyesho hayo ya kazi za ubunifu kwa masomo ya sayansi

 Baaddhi ya shule hizo ni Kinondoni, Kambangwa, Bunge Olimpio, Bunguruni Malapa na  nyingine lengo likiwa ni kujaribu kuwakutanisha wanafunzi wenye mitizamo tofauti na wenye uwezo

Akifafanua zaidi alisema shule ya Academic inampango ya kufadhili wanafunzi wtakaofanya vizuri katika masomo ya sayansi hivyo maonyesho haya yanaweza wanufaisha wanafunzi wanaosoma shule za kawaida za serikali .

 Nae Mwanafunzi wa shule ya Bungoni  alisema wao wamefurahi kuungana na wanafunzi ambao wanasoma michepuo ya kingereza lakini tulipofika katika swala la ubunifu woote tumekuwa tunaongea kitu kimoja tofautio yao na sisi wao wanauwezo wa kuongea Kingereza Zaidi yetu sisi tunaesoma katika shule za michepuo ya Kiswahili lakini nitajitahidi mwakani nishiriki kubuni kitu ili nipate ufadhili wa kusoma katika shule hizi.

Alli Sajjd akionyesha Robot la Umeme alilotengeneza kwa makatarasi na plastic  kwa kutumia mfumo a umeme Jua wakati wa  Mwanafunzi wa shule ya Academic achievement open school jijini Dar es salaam .
Khalid Ramadhan  Mwanafunzi wa shule ya Academic Achievement Open School akielezea jinsi alivyoweza kubuni na kutengeneza feni ya maboks kwa kutumia mfumo wa umeme  na mabaki ya mabetri chakavu wakati wa maonyesho ya sayansna Ubunifu kwa wanafunzi wa shule  msingi na sekondari .
Mwanafunzi wa shule ya Academic achievement open school,Sumaiya Abdullwahd   akielezea jinsi alivyoweza kutengeneza mfumo wa umeme kwa kutumia betri na  na mionzi ya jua kwa wanafunzi ikiwa ni jaribio la sayansi wakati wa Maonyesho ya vipaji kwa masomo ya Sayansi yaliofayika shulerni kwao jijini Dar  Salaam jana.
Mwanafunzi wa shule ya Academic achievement open school,Malaika Sikandar   akielezea jinsi alivyoweza kutengeneza mfumo wa umeme kwa kutumia mabaki ya betri na kuweza kuwasha taa  kwa wanafunzi ikiwa ni jaribio la sayansi wakati wa Maonyesho ya vipaji kwa masomo ya Sayansi yaliofayika shulerni kwao jijini Dar  Salaam.
Kamati ya maandalizi ikiwa katika picha ya pamoja baada ya kufanikisha mashindano hayo


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...