*Vijana wanapata ulaghai wa watumiaji wa mitandao wasiowaadilifu kwa kupatiwa taarifa za siri katika mitandao yao
Na Chalila Kibuda,Michuzi TV
MAMLAKA
ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),imesema baadhi ya watumiaji wa mitandao
wamekuwa wakiwalaghai vijana na kuwasababishia madhara mbalimbali ya
katika utumiaji wa mitandao
Hayo
ameyasema Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt.Jabiri Bakari
ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya leseni wa Mamlaka hiyo John Daffa
wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni 2022 yaliyofanyika
jijini Dar es Salaam.
Daffa
ametoa onyo kwa wale wanaotumia mitandao vibaya na kusema sheria
ziwepo huku wengine wakishitakiwa kutokana na kutumia mitandao hiyo .
Daffa
amesema uwezo wa mtandao kuficha utambulisho wa mtumiaji, umewawezesha
watu wenye nia ovu kujifanya kama vijana wadogo na kushawishi vijana
kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi katika umri mdogo hivyo TCRA
imekuwa sehemu ya wajibu wa kutoa elimu kwani matumizi ya Internet ni
ushiriki jumuishi.
'"Vile
vile watu hao wanaweza kuiba au kukushawishi uwatumie taarifa zako
binafsi kama picha,nywila pamoja na mwaka wa kuzaliwa kuzitumia
kufanya uhalifu mtandaoni ikiwa ni pamoja kufanya utapeli, kusambaza
taarifa za uongo wakilenga kuchafua taswira yako au kufanya manyanyaso
dhidi yako na kusababisha usumbufu kwa waathirika wa vitendo hivyo
hivi,"amesema Daffa
Amesema
pamoja na mitandao ya kijamii kuwa nyenzo za kulinda usiri vijana wengi
hawatumii nyenzo hiyo na hivyo kusababisha taarifa zao kuonekana kwa
watu wenye nia mbaya na hivyo kuzitumia vibaya dhidi yao na kujikuta na
wanaathirika kisaikolojia.
Akitoa takwimu alisema hadi Disemba mwaka Jana idadi ya watumiaji wa mtandao wa intaneti imekuwa hadi
mawasiliano kukua.
Daffa
amesema huduma za mawasiliano zitumike kwa kuhabarisha pamoja na
kufungua fursa za kibiashara katika mitandao kwa kuuza bidhaa za aina
mbalimbali na kusaidia nchi kuendelea kukua kiuchumi.
Amesema
serikali imejipanga vyema kuandaa mazingira bora na wezeshi kwa jamii
ya watanzania kushiriki ipaswavyo kwenye uchumi wa kidijitali kwa wazazi
na watoto ili kuwa na mnyororo wa kutumia mitandao kwa usalama.
"
Tumeshuhudia watu wengi wakiinuka kiuchumi kwa kutumia mtandao. Wengi
wanaweza kufanya biashara na kuinua maisha yao wenyewe na wale
waliowaajiri ikiwa ni pamoja na kuchangia kwenye pato la
taarifa,'alisema.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano ( Tehama), Connie Francis alisema Tanzania ni moja ya nchi
iliyochukua hatua katika matumizi ya tehama na kuwa shirikishi.
Maadhimisho
ya Siku hii ni mango wa kimataifa ulioanzishwa 2014 kwa lengo la
kuhamasisha matumizi bora na salama ya mtandao wa intaneti.
Mwanafunzi
wa Shule ya Sekondari Chang'ombe Demostration Husna Ramadhan amesema
kupata elimu ya matumizi ya mitandao ni nzuri kwani baadhi ya vijana
wanaigia kutumia vibaya kutokana na kukosa elimu hiyo.
Amesema
kuwa sheria zieongezwe kuwabana watumiaji wa mitandao ili wasiweze
kuharibu jamii na elimu endelee kutolewa na wanafunzi wa elimu ya msingi
ili wakifika katika umri wa kumiliki simu au komputa wanakuwa na uelewa
juu ya matumizi ya mitandaoPicha
mbalimbali za pamoja wanafunzi wa Shule za Msingi,Sekondari na Vyuo na
Meza kuu katika maadhimisho ya siku ya usalama matandao yalifanyika
jijini Dar es Salaam.
Washindi wa Mashindano ya Tehema wakiwa na Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya siku ya usalama mtandaon yaliyoanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Tehama wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Connie Francis akizungumza kuhusiana na TCRA inavyotoa mafunzo juu ya Tehama pamoja na kuandaa mashindano mbalimbali ,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Leseni wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) John Daffa akizungumza wakati maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Washindi wa Mashindano ya Tehema wakiwa na Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya siku ya usalama mtandaon yaliyoanyika jijini Dar es Salaam.
Washindi wa mashindano ya Tehama yaliyoendeshwa na TCRA wakiwa na vyeti vyao katika maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni.
Meneja
wa Huduma za Watumiaji huduma za Mawasiliano Thadayo Ringo akizungumza
kuhusiana na huduma za mawasiliano kwa wanafunzi katika maadhimisho ya
siku ya usalama mtandaoni ambayo huadhimishwa kila Desemba 8 Duniani
yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.Mkurugenzi wa Idara ya Tehama wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Connie Francis akizungumza kuhusiana na TCRA inavyotoa mafunzo juu ya Tehama pamoja na kuandaa mashindano mbalimbali ,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Leseni wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) John Daffa akizungumza wakati maadhimisho ya Siku ya Usalama Mtandaoni yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...