Na. John Mapepele

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe Pauline Gekul amewakaribisha wadau mbalimbali kushiriki kwenye tamasha Kubwa la Muziki la Serengeti liliolatibiwa na Wizara yake litakalofanyika jijini Dodoma Machi 12-13,2022 jijini Dodoma.

Wito huo ameutoa wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani Machi 8, 2022 kwenye Tamasha la aina yake la Orange Concert na harambee ya uchangiaji wa Timu ya Taifa ya wanawake(Twiga Stars) ambapo zaidi ya milioni 377 zilichangishwa.

Tamasha hilo lililoenzi ubunifu wa sekta za sanaa na michezo ambapo taasisi ya wasanii ya Dadahood na Baraza la Michezo Tanzani ziliungana pamoja na mambo mengine kutumia sanaa kuwachangia Twiga Stars.

Katika tamasha hilo mbali na wasanii mbalimbali kutoa burudani za kutosha kikundi cha hamasa cha wizara ya utamaduni, sanaa na michezo kilimetia fora katika mtindo wake wa kutumbuiza ambapo awali kilikaa nje ya ukumbi na kuwakaribisha wageni kwa matarumbeta.

Kikundi hiki kimeundwa na watumishi na wataalam wa utamaduni na sanaa ambapo kimekuwa kikitoa hamasa kubwa inayowavutia wengi kwenye shughuli na matamasha yanayoandaliwa na Wizara kama mashindano ya soka ya Bara la Afrika kwa wenye ulemavu (CANAF) na mashindano ya Taifa CUP.

Katika tamasha hilo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alituma ujumbe wa kuchangia milioni 10 kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo. Baada ya muda Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naye kupitia kwa Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Mchemba, akapiga simu na kuchangia milioni 15.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...