Na Pamela Mollel,Arusha

Jamii imeshauriwa kutumia kwa wingi Mchicha lishe wa Akeri uliofanyiwa utafiti wa kina na Taasisi ya utafiti wa kilimo(TARI-Tengeru)na kugundulika kuwa na virutubisho vingi hasa madini ya Zinki ili kuondokana na tatizo la udumavu

" Kwa wanaume wenye changamoto ya tendo la ndoa mchicha huu unasaidia kuimarisha majukumu yao ikiwemo kuboresha mfumo wa uzazi"

Akizungumza hivi karibuni na waandishi wa habari jijini Arusha,waliopatiwa mafunzo na Tume yaTaifa ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH)Mtafiti Mwandamizi Emmanuel Lasway kutoka TARI alisema Mchicha huo umepewa kipaumbele kwa sababu unaweza kutumia majani na mbegu

Alisema kuwa kwa sasa wanashauri jamii hasa wanaume kutumia nafaka ya Mchicha wa Akeri kutokana na namna ambavyo umefanyiwa utafiti na kugundulika unaprotini 14.5%huku ukiwa ni chanzo bora cha vitamini A,B,Zinki,madini ya chokaa,chumvi na folikasidi

Mtafiti huyo aliongeza kuwa Mchicha huo wa maajabu huvunwa shambani na kisha mbegu zake husagwa na kuchanganya kwenye vyakula ili kuongeza virutubisho

"Unga wa Mchicha huchanganywa kwenye unga waugali,vitafunwa,uji,shurubati na vyakula vingine ili kuongeza virutubisho "alisema Lasway

Hata hivyo Mchicha huu unatajwa kuwa na protini nyingi zaidi ya mahindi na ngano

"Mchicha lishe huu unachangia kiasi cha 50-102%folikasidi ukilinganisha na mahindi 15-46%na ngano 20-51%"alisema Lasway

Pia Mchicha huu unatajwa kuwa ni mzuri kwa ukuaji watoto na wajawazito

Ukosefu wa kula mboga na matunda husababisha ukosefu wa damu,udumavu na uoni hafifu

Uzalishaji wa mbegu ulianza rasmi 2018 ambapo kwa sasa mbegu hizo hupatikana kituo cha TARI Tengeru na wakala wa mbegu (ASA)

Mafunzo ya siku 4 ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari yaliyofadhiliwa na COSTECH yalilenga kuwajengea uwezo waandishi kuandika habari za Sayansi na Teknolojia

Picha ikionesha Mchicha wa Akeri uliofanyiwa utafiti wa kina

Mtafiti Mwandamizi kutoka Taasisi ya utafiti wa kilimo TARI-Tengeru Emmanuel Lasway akielezea maajabu ya Mchicha huo wa Akeri
Mbegu za Mchicha wa Akeri kabla haujasagwa na kuwa unga,unga huu unatajwa kuwa na virutubisho vingi kwa afya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...