Mkurugenzi wa Miundombinu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Mhandisi Faustine Kataraiya, akifafanua jambo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Selemani Kakoso (wa tatu Kulia) pamoja na wajumbe, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa Kiwanda cha mataruma cha reli ya Kisasa ya SGR, Sehemu ya Mwanza-Isaka (KM 342) kinachojengwa Wilayani Kishapu, Mkoani Shinyanga.



Meneja Mradi wa Mradi wa Reli ya Kisasa ya SGR, Sehemu ya Mwanza-Isaka (KM 341), Mhandisi Masanja Machibya akifafanua kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Selemani Kakoso (Kulia) na wajumbe wa kamati kuhusu hatua mbalimbali za ujenzi wa Kiwanda cha mataruma cha reli ya Kisasa ya SGR, kinachojengwa Wilayani Kishapu, Mkoani Shinyanga, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi huo mwishoni mwa wiki.



Meneja Mradi wa Mradi wa Reli ya Kisasa ya SGR, Sehemu ya Mwanza-Isaka (KM 341), Mhandisi Masanja Machibya akifafanua kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Selemani Kakoso (Kulia) na wajumbe kuhusu Kiwanda cha mataruma cha reli ya Kisasa ya SGR kupitia michoro, kinachojengwa Wilayani Kishapu, Mkoani Shinyanga, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi huo mwishoni mwa wiki.



Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso akitoa maelekezo kwa Uongozi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), wakati Kamati hiyo ilipotembelea Mradi wa Reli ya Kisasa ya SGR, sehemu ya Mwanza-Isaka (KM 264) eneo la Seke, Wilayani Kishapu, Mkoani Shinyanga.



Muonekano wa kipande cha Reli ya Kisasa ya SGR, Sehemu ya Mwanza-Isaka (KM 341) kilichotandikwa katika eneo la Seke, Wilayani Kishapu, Mkoani Shinyanga.



Muonekano wa hatua za awali za ujenzi wa Kiwanda cha mataruma cha reli ya Kisasa ya SGR, kinachojengwa Wilayani Kishapu, Mkoani Shinyanga. Kiwanda hicho ni sehemu ya mradi wa Mwanza-Isaka (KM 341) ambapo ujenzi wake mradi umefikia asilimia 4.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...