Na Amiri Kilagalila,Njombe
Wakati zoezi la ukusanyaji wa taarifa za mfumo wa anwani za makazi na postikodi likiendelea kote nchini,Kamisaa wa Sensa ya watu na makazi kutoka serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Balozi Mohamed Haji Hamza ametoa agizo kwa wakusanya taarifa za makazi na makarani kote nchini kuifanya kazi hiyo kwa umakini kwa kuwa zoezi hilo linabeba mipango ya muda mrefu ya serikali.
Balozi Mohamed Haji Hamza amesema hayo wakati alipokutana na katibu tawala wa Mkoa wa Njombe, Judica Omari ofisini kwake kwa ajili ya maandalizi ya uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa na kusema mbio za mwenge wa uhuru mwaka huu zimelenga kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhesabiwa.
“Hapa tupo na vitu viwili kwa maana mkoa umebeba hili la mwenge kwasababu sehemu kubwa ya ujumbe wa mwenge itakuwa na sense ya watu na makazi”alisema Balozi Mohamed Haji Hamza
Akizungumza namna serikali ilivyojipanga kufanikisha zoezi la Sensa ya watu na makazi kwa kiwango cha juu Balozi Mohamed Haji Hamza amesema.
“Tunahitaji kuwa na nguvu za pamoja kuweza kuhamasisha na kueleimisha wananchi ili waweze kukubali kuhesabiwa siku ya sensa”
Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Judica Omari amesema wakati mkoa umejiandaa kikamilifu kushiriki uzinduzi wa mbio za Mwenge suala la kufanyika kwa sensa ya watu na makazi nalo lina umuhimu mkubwa katika kuwaletea maendeleo wananchi.
“Tunajua swala hili litasaidia kwa kuwa maendeleo yetu sasa tunayoyapanga,yanaenda kupangwa kwa usahihi zaidi kutokana na takwimu tutakazo kuwa nazo zitakuwa za uhakika zaidi”
Wakati serikali ikihimiza utekelezaji wa zoezi hilo, Mkuu wilaya ya Njombe Kissa Kasongwa amezindua mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo wa kukusanya taarifa za mfumo wa anwani za makazi na postikodi kwa makarani katika halmashauri ya mji wa Njombe.
Kamisaa wa Sensa ya watu na makazi kutoka serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Balozi Mohamed Haji Hamza akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Njombe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...