NAIBU Waziri Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora, Deo Ndejembi amewataka Waratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) Mkoa wa Mwanza kusimamia kwa uadilifu miradi 104 yenye thamani ya Sh Bilioni 7.8 itakayotekelezwa ndani ya Mkoa huo.

Ndejembi ametoa kauli hiyo leo jijini Mwanza wakati alipokua akizungumza na watendaji wa TASAF Mkoa huo ambapo aliwataka kusimamia miradi hiyo kwa uzalendo huku pia akiwataka Waratibu hao kuwashirikisha viongozi wa Wilaya na Mkoa kwenye kila mradi unaotekelezwa na TASAF.

"Ndugu zangu Rais Samia ametoa Sh Bilioni 7.8 kwenye Mkoa huu pekee kwa ajili ya utekelezaji wa miradi 104 ambayo imepitishwa na Wizara. Miradi 31 ya Afya, Miradi 49 ya Elimu na Miradi 24 ni ya kutoa ajira za muda.

Miradi Hii itatekelezwa kwenye Halmashauri zote nane za Mwanza, hakikisheni inakamilika kwa wakati na thamani ya fedha ionekane, kama kuna mtu anafikiria hizo fedha ajue zitamtokea puani, hatutoruhusu ubadhirifu wowote utokee na TAKUKURU niwatake muwe macho kwenye ujenzi wa miradi Hii yote," Amesema Ndejembi.

Naibu Waziri Ndejembi pia amewataka Waratibu hao kuwashirikisha viongozi wengine juu ya utekelezaji wa miradi hiyo ili waweze kuifahamu na kuifanyia ufuatiliaji pindi inapokua inatekelezwa.

" Msifanye miradi bila kuwashirikisha viongozi, Wakuu wa Wilaya na Wabunge, wao pia ndio wenye kujua mahitaji haswa ya wananchi wa eneo husika, nyie mnaweza kusema hapa paletwe kituo cha Afya kumbe Mbunge alishaomba Serikalini na akaahidiwa atapatiwa sasa mkishauriana inakua ni vizuri maana yake mtapang kwa pamoja jambo la kufanya ambalo litawanufaisha wananchi," Amesema.

Kwa upande wake Mratibu wa TASAF Mkoa wa Mwanza, Monica Mahundi amesema TASAF awamu ya tatu imekua na mafanikio makubwa ambapo Kaya zilizotambuliwa na kuandikishwa kwa kuzingatia vigezo zinaendelea kupokea malipo ya ruzuku, Kaya nufaika zina uhakika wa kula milo miwili au mitatu tofauti na awali kwa asilimia 92 na Walengwa 38,804 wameanzisha shughuli za kujiongezea kipato ambazo ni Kilimo, Ufugaji na Biashara ndogo ndogo.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deo Ndejembi akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Mwanza na Waratibu wa TASAF Mkoa huo kwenye kikao kazi chake na Waratibu hao.


Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deo Ndejembi akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Ngusa Samike, Wakuu wa Wilaya za Ilemela na Magu na baadhi ya wawakilishi wa TASAF Makao Makuu mara baada ya kumaliza kikao kazi na Waratibu wa TASAF Mkoa wa Mwanza.
Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa TASAF, Sarah Mshiu akizungumza na Waratibu wa TASAF Mkoa wa Mwanza wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deo Ndejembi na watumishi hao leo Jijini Mwanza.
 
Waratibu wa TASAF Mkoa wa Mwanza wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deo Ndejembi alipofika kuzungumza nao Jijini Mwanza leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...