Na Pamela Mollel,Arusha

Mradi mkubwa wa upanuzi wa bandari ya Tanga umefikia asilimia 26 wa ujenzi wake huku ukitarajiwa kukamilika Oktoba mwaka huu

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika maonesho ya TANZFOOD,Mhandisi Hamis kipalo alisema mradi huo upo nyuma ya muda kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya ugonjwa wa Covid 19 iliyosababisha nchi nyingi kufunga mipaka

"Ugonjwa wa Covid 19 ulisababisha vifaa vya ujenzi kutoingia nchini kutokana na nchi nyingi kufunga mipaka yao"alisema Mhandisi Kipalo

Aliongeza kuwa mradi huo ukikamilika utaleta manufaa makubwa kwa nchi katika kuongeza ufanisi wa bandari kutoka tani laki saba na nusu hadi tani Milioni 30

"Uwezo wa bandari utaongezeka na pia itasaidia biashara katika ukanda wa kaskazini na Afrika Mashariki "alisema Mhandisi Kipalo

Naye Afisa uhusiano wa bandari ya Tanga,Adam Shindo alisema ushiriki wao katika maonyesho hayo ni kusogea karibu na wateja wao nakutumia fursa hiyo kwa kujitangaza zaidi

"Kilichotuleta hapa ni kusogea karibu na wateja wetu na kuwaelezea maendeleo ya mradi,upanuzi wa bandari ya tanga "alisema Shindo

Mradi huo unatekelezwa na kampuni ya CHEC kutoka China na kusimamiwa na Mhandisi mshauri kutoka Denmark ikishirikiana na kampuni ya Kitanzania Anova

Afisa uhusiano wa bandari ya Tanga Adam Shindo akizungumza na vyombo vya habari katika maonyesho ya kimataifa TANZFOOD jijini Arusha

Mhandisi Hamisi Kipalo akizungumza na waandishi kuhusu maendeleo ya mradi mkubwa wa upanuzi wa bandari ya Tanga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...