Na Fredy Mshiu
Kamati
 ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji imeridhishwa na usimamizi na 
utekelezaji wa miradi ya Maji ya Kibamba-Kisarawe na Pugu-Gongo la mboto
 iliyotekelezwa na DAWASA kwa kupitia fedha za ndani.
Akiongea
 wakati wa ziara ya kamati hiyo kwenye miradi ya maji Jijini Dar es 
salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge Mhe. Jerry Silaa (Mb) 
amesema hali ya usambazaji maji katika Jiji la Dar es salaam na Mkoa wa 
Pwani  inaridhisha hususani katika maeneo yaliyokuwa sugu na upatikanaji
 wa Maji kama vile Kisarawe na Pugu.
"Mfano
 mzuri ni hapa tulipo katika jimbo la Ukonga, ambapo kwa takribani miaka
 40 hapakuwepo huduma ya majisafi, lakini utekelezaji wa mradi wa 
Pugu-Gongo la mboto umemaliza changamoto hiyo iliyodumu kwa muda 
mrefu".ameleeza Mh.Slaa
Mheshimiwa
 Slaa ameongeza kuwa kwa kasi wanayoenda nayo DAWASA kamati inaamini 
ifikapo 2025 itakuwa imewafikia Wananchi wote katika eneo lake la 
kihuduma.
Kwa
 upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu DAWASA  Mhandisi Cyprian Luhemeja 
ameeleza kuwa kazi kubwa imefanyika na inaendelea kufanyika, katika  
usambazaji wa maji ili kuhakikisha yanawafikia wananchi wote.
"Tulipokea
 Maelezo kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh.Samia 
Suluhu Hassan kuharakisha usambazaji wa maji kwa wananchi katika maeneo 
 ambayo miradi imekamilika. Lakini pia tumepokea maelekezo ya Kamati 
katika kuharakisha usambazaji wa huduma ya maji na tunaenda kutekeleza 
hilo kwa kasi".ameeleza Mhandisi Luhemeja.
Ndugu
 Bakari Utingo, mkazi wa Kata ya Majohe ameishukuru DAWASA kwa kufikisha
 huduma ya maji katika kata zote za Pugu na kwa sasa maji ni Mengi na ya
 uhakika.
"Nakumbuka
 Mara ya mwisho maji kutoka bombani katika kata yetu ya Majihe ni mwaka 
1999, tumekuwa tukitumia maji ya visima na kununua kwa watoa huduma 
binafsi kwa muda mrefu. Tunashukuru sasa tumefikishiwa huduma na 
DAWASAna niwaombe waendelee na kasi ya kuunganisha huduma ya maji kwa 
wananchi wengi zaidi".ameeleza Utingo
DAWASA inatekeleza miradi mikubwa na midogo mbalimbali ili kufikia asilimia 95 ya upatikanaji ifikapo 2025.
 





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...