Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Dk.Damas Ndumbaro (Mb), Waziri wa Maliasili na Utalii pamoja na Samwel W. Shelukindo ambaye ni Balozi wa Tanzania nchini Uhispania mwenye makazi yake mjini Paris, Ufaransa wamefanya mazungumzo na vilabu vya Atlético de Madrid na Getafe FC.

Vilabu hivyo vinashiriki ligi kuu ya Uhispania (Laliga), pia wamefanya mazungumzo na timu inayotarajia kupanda daraja ya Real Valladolid, inayomilikiwa na mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Ronaldo De Lima.

Lengo la mazungumzo hayo, lilikuwa kushawishi timu hizo kuitangaza Tanzania kiutalii ili kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea Tanzania.

Timu hizo ambazo zinaangaliwa na idadi kubwa ya watazamaji sio tu nchini Uhispania, bali pia duniani kwa ujumla, zimeonyesha utayari wa kuitangaza Tanzania kiutalii.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Damas Ndumbaro (Mb), akiwa katika mkutano na uongozi wa timu ya Getafe inayoshiriki daraja la kwanza (Laliga) ya Uhispania. Kushoto kwa Mhe. Waziri, ni Mhe. Samwel W. Shelukindo, Balozi wa Tanzania nchini Uhispania mwenye makazi yake mjini Paris, Ufaransa.

Mhe. Waziri Damas Ndumbaro (Mb), Waziri wa Maliasili na Utalii (kushoto) akiwa na Mhe. Balozi Samwel W. Shelukindo, Balozi wa Tanzania nchini Uhispania mwenye makazi yake mjini Paris, Ufaransa, wakiwa wamesimama nyuma ya sanamu la mchezaji aliyevaa jezi inayoitangaza Tanzania
Ujumbe wa Tanzania ukiwa katika mkutano na uongozi wa timu ya Atlético de Madrid


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...