Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) Dk. Adelhelm Meru akipewa kadi ya NHIF   kutoka kwa Meneja Uhusiano wa NHIF Anjela Mziray wakati  alipotembelea Banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika Maadhimisho ya Siku ya Usalama Mahala Pa Kazi yaliyofanyika Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) Dk. Adelhelm Meru akizungumza na waandishi wa Habari wakati alipotembelea Banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika Maadhimisho ya Siku ya Usalama Mahala Pa Kazi yaliyofanyika Jijini Dodoma.

Na Mwandishi Wetu
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakala Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) Dk.Adelhelm Meru ameshuhudia namna Kadi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya inavyomsaidia yeye na familia yake katika kupata huduma za matibabu.

Amesema bila kuwa na Kadi hiyo angekuwa na mzigo mkubwa sana katika eneo la matibabu hivyo amewaomba wananchi kutofanya mchezo katika kuamua kujiunga na NHIF.

Hayo ameyasema leo wakati alipotembelea banda la NHIF katika viwanja vya CCM Jijini Dodoma kwenye Maonesho ya Wiki ya Usalama Mahala pa Kazi ambapo Mfuko unatoa huduma mbalimbali ikiwemo ya elimu na uandikishaji wa wanachama.


Ameongeza kuwa kadi ya NHIF imekuwa na heshima kubwa katika vituo vyote vya kutolea huduma na kwa sasa imeondoa mitazamo hasi ya kunyanyapaliwa kwa wanachama wa Mfuko.


“Nawasihi sana wananchi wasifanye mchezo na eneo la kujiunga na NHIF kwa sababu maisha ya sasa bila kuwa na bima ya afya ni ngumu sana kumudu gharama za matibabu,” alisisitiza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...