Na Zuena Msuya, Lindi

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali ametembelea na kukagua eneo la Likong’o litakalojengwa Mradi wa kusindika Gesi Asilia (LNG) na eneo la makutano ya kuunganisha gesi inayotoka mkoani Mtwara na Songosongo mkoani Lindi.

Akiwa katika ziara hiyo amewaasa watendaji wa maeneo hayo kutekeleza majukumu yao kwa weledi kwa kuzingatia manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla.

Katika ziara hiyo ya kikazi, Mahimbali aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga, Kamishna Msaidizi wa Mafuta na Gesi kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Mohamed Fakih, na Meneja wa Kiwanda cha kuchata gesi asilia cha Madimba, Mhandisi Sultan Pwaga, pamoja na maafisa wengine kutoka wizarani na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC). Ziara hiyo imefanyika Aprili 2, 2022 mkoani Lindi.

Ziara hiyo ni muendelezo wa ziara yake aliyoianza Machi 31, 2022 kwa kukagua mradi wa gesi wa Songosongo mkoani Lindi, kisha Aprili 1, 2022 alikagua kiwanda cha kuchakata gesi asilia cha Madimba, visima vya gesi katika eneo la Mnazi Bay pamoja mradi wa usambazaji wa miundombinu ya gesi asilia kwa matumizi ya kupikia majumbani. 








Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali (wa kwanza kushoto), akitoa maelekezo kwa Watedaji wa Wizara hiyo na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), alipowasili katika eneo litakalojengwa mradi wa kusindika gesi asilia (LNG), Likong’o Mkoani Lindi



Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali (kulia) akionyeshwa mchoro wa ramani ya eneo litakalojengwa mradi wa kusindika gesi asilia (LNG), na Mjiolojia mwandamizi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Simon Zabron, wakati wa ziara ya kukagua eneo hilo lililopo Likong’o Mkoani Lindi,



Kamishna msaidizi wa Mafuta na Gesi wa Nishati nchini, Mhandisi Mohammed Fakih akifafanua jambo kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali (wa pili kulia), wakati wa ziara ya kukagua eneo hilo lililopo Likong’o Mkoani Lindi,



Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali, akikagua sehemu ya mabomba ya gesi asilia katika kituo cha makutano ya kuunganisha gesi hiyo inayotoka Mtwara na Songosongo Mkoani Lindi, mara baada ya kutembelea kituo hicho kilichopo katika Kijiji cha Somangafungu Mkoani Lindi Aprili, 02, 2022.



Muonekano wa sasa wa eneo litakalojengwa mradi wa kusindika gesi asilia (LNG) lililopo Likong’o Mkoani Lindi, Aprili,


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...