Na Mwamvua Mwinyi,Chalinze
Baadhi ya wananchi wa jimbo la Chalinze,wanamtakia kheri ya siku ya kuzaliwa mbunge wa Jimbo Hilo Ridhiwani Kikwete ambae pia ni Naibu Waziri wa Ardhi .
Ridhiwani Kikwete amezaliwa miaka kadhaa iliyopita , April 16 ambapo wananchi wake wamemtakia maisha marefu yenye afya ili aendelee kuwaongoza.
Kwa upande wake Ridhiwani anasema Utu Uzima unamnyemelea sasa!!! Anamshukuru Allah tena kwa Mwaka mwingine. Kwa hakika ni majaliwa yake yanayomfanya awe miongoni kwa aliowapendelea katika Dunia hii.
"Niwe mwenye bahati ni kwa ajili yako Allah"." Nakushukuru siku zote na hata inapoingia siku hii ni kwa Uamuzi wako ninashereheka. Asante Allah kwa Umri Mwengine.#HappyBirthdayToMe"
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...