Na Janeth Raphael - DODOMA

RAIS Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya sherehe za mei mosi ambayo Kitaifa yatafanyika katika uwanja wa jamhuri jijini Dodoma.

Akizungumza na wandishi wa habari jm Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Antony Mtaka amesema kabla ya kilele kutatanguliwa na shughuli mbalimbali ikiwemo maonyesho, michezo na makongamano.

"Nimekutana nanyi leo kuwafahamisha kuwa kwa mwaka huu Mkoa wa Dodoma umepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa sherehe za mei mosi  Kitaifa ambapo zitaambatana na shughuli mbalimbali katika juma la maadhimisho kabla ya kilele ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rasi Samia,"amesema

Mtaka ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi wa sherehe hizo alisema alikutana na wahariri wa vyombo vya habari ambao aliwafahamisha kuhusu heshima ambayo Mkoa umepata na kuwashirikisha kuhusu namna bora ya kuwa na kampeni ya hamasa lengo ni kufanya mei mosi ya mwaka huu ifanyike kivingine.

Amesema Mkoa umeandaa kampeni maalumu ya vyombo vya habari Kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kushiriki Kwa wingi katika sherehe hizo na kutumia fursa ambazo zitapatikana kupitia shughuli mbalimbali zitakazofanyika kabla ya kilele.

"Ndugu zangu shughuli hii ni yetu sote kwahiyo tutumie fursa hii kutangaza Mkoa wetu ambao ni makao makuu ya nchi lakini pia shughuli zitakazofanyika ni pamoja na kikao na wahariri, uzinduzi wa hashtag, michezo ikiwemo mpira wa miguu,Pete,kikapu na maonyesho mbalimbali ambayo yataanza April 22 hadi 30 mwaka huu katika viwanja vya Jakaya Kikwete,"amesema.

Katika hatua nyingine Mtaka alisema Mkoa umeandaa nukuu mbalimbali za viongozi zilizowahi kutolewa katika maadhimisho  mbalimbali ya sherehe za mei mosi.

Kwa upande wake Rais wa Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi (TUCTA) Tumaini Nyamhokya ameema sherehe za maadhimisho ya mei mosi Kwa mwaka huu zitakuwa kivingine kwani Hadi Sasa maandalizi yamefikia katika hatua ya kuridhisha.

Alishauri wataalamu wanaohusika na kutoa elimu ya Sensa ya Watu na Makazi kutumia fursa hiyo kutoa elimu kupitia mikusanyiko ya watu watakaokuja kushiriki ikiwemo katika makongamano na maonyesho.

"Tunashukuru sana uongozi wa Mkoa wa  Dodoma Kwa kutoa ushirikiano wa kutosha na tunawahakikishia wafanyakazi kuwa sherehe za mwaka huu zitakuwa kivingine, pia hii ni fursa Kwa watu wa sensa ya watu na makazi kutumia fursa hii kutoa elimu Kwa wananchi kuhusu umuhimu wa sensa ili watu wakae tayari kuhesabia,"amesema

Naye Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kati Jane Maganga aliwataka wananchi kujitokeza Kwa wingi katika maonyesho na makongamano yatakayofanyika kwàajili ya kupata elimu kuhusu mikopo ambayo inatolewa na benki hiyo Kwa wafanyabiashara wadogo.

Amesema katika sherehe hizo benki ya CRDB ndio mzamini mkuu na wataendelea kushirikiana na serikali katika kutoa huduma Kwa wananchi ikiwemo utoaji mikopo ili kuboresha maisha.

"Tunapenda kuwaalika wananchi kujitokeza Kwa wingi kushiriki katika shughuli mbalimbali ambazo zitafanyika kabla ya kilele cha meimosi na sisi kama CRDB  tukiwa kama wadhamini wakuu tumejipanga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma zetu ambazo zimeboreshwa,"amesema.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...