Na Amiri Kilagalila,Njombe 
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Hassan Suluhu ametuma salamu 
za pole kwa wafiwa kutokana na vifo vya watu 9 waliofariki kwa ajali ya 
gari mkoani Njombe. 
Akitoa salamu hizo kwa niaba ya Rais katika 
ibada ya kuaga miili hiyo katika kanisa la mtakatifu Joseph jimbo 
Katoliki Njombe mkuu wa mkoa wa Njombe Waziri Kindamba ametoa wito kwa 
waombolezaji kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu. 
“Lakini
 pia napenda kuchukua nafasi hii kutoa salamu za pole kutoka kwa Rais wa
 jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ambaye naye 
ameguswa sana na msiba huu”alisema Waziri Kindamba. 
Kwa upande 
wake mhashamu Askofu John Chrisostom Ndimbo wa jimbo Katoliki la Mbinga 
na msimamizi wa kitume wa jimbo katoliki la Njombe ametoa shukrani kwa 
serikali,jeshi la polisi pamoja na madaktari kutokana na ushirikiano 
mkubwa waliouonyesha katika kipindi hiki kigumu kwao. 
“Nikushukuru
 mkuu wa mkoa ulikuwa mstari wa mbele kwa niaba ya serikali ya Tanzania 
uliposkia taarifa za ajali hiyo,ukakimbia mahospitalini kuwaona lakini 
pia ukakimbia katika sehemu ya ajali”alisema mhashamu Askofu John 
Chrisostom Ndimbo 
Watu hao ambao ni kutoka umoja wa vijana 
Katoliki Njombe (UVIKANJO) walifariki kwa ajali ya gari tarehe 24 katika
 eneo la Igima kibaoni walipokuwa wakitoka 
kutembelea kituo cha kulea watoto yatima kilichopo Ibumila wilayani Njombe.


 

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...