Na Mwamvua Mwinyi,Pwani


Mkuu wa Mkoa wa Pwani, alhaji Abubakar Kunenge ameuagiza uongozi wa Chama kikuu Cha Ushirika Mkoani Pwani  CORECU kuwachukulia hatua Kali za kisheria wale watakaobainika  kuhujumu Chama hicho.

Sambamba na Hilo,  ameupongeza uongozi wa mpito wa Chama hicho Kwa  kusimamia zao la korosho ambapo uzalishaji umeongezeka kutoka Tani 7  mwaka 2019/20 Hadi kufikia Tani 15  msimu wa  mwaka 2021/22 na Daraja la kwanza la korosho kufikia Tani 72 ya Korosho zote.

Aliyaelekeza hayo, katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka  wa Chama hicho uliofanyika mjini Kibaha April 21,2022 katika ukumbi wa Shirika la Elimu Kibaha.

Kunenge alikitaka Chama hicho kiwe na utaratibu wa kuwajibishana endapo kiongozi ama Mwanachama anaenda kinyume na taratibu za Chama hicho.

Pia amewataka wakuu wa Wilaya kuwachukulia hatua  ,wanaoenda kinyume bila kujali itikadi za Chama.

Katika hatua nyingine RC Kunenge Amesema mkoa na Wilaya umedhamiria kuleta mapinduzi katika Zao la Korosho.

"Tumedhamiria kuleta Mabadiliko katika Zao hilo la korosho ila peke yetu hatuwezi ni lazima tushirikiane katika hili."alifafanua.

Vilevile aliwataka Wanachama wa CORECU wasifanye makosa katika kuchagua viongozi wapya baada ya uongozi wa mpito kumaliza muda wake.

Alisema endapo Chama hicho kikipata viongozi waadillifu ,wasimamizi Wazuri na watakaotosha Basi kitafanya vizuri katika majukumu yake.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...