Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge,ameingilia kati mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wavamizi pamoja na moja ya familia ambayo ndio wamiliki halali wa eneo huko Kitongoji Cha Sanzale Kata ya Magomeni, Bagamoyo.

Akiwa katika eneo lenye mgogoro aliwataka  wananchi hao, kuhakikisha wanalipa fidia ya eneo hilo kwa kufuata makubaliano yaliyotolewa na familia.

Aidha , amemuagiza Mkuu wa Wilaya hiyo Zainabu Abdallah kuhakikisha anaendesha msako wa  kuwakamata matapeli wote waliohusika katika eneo hilo ili wachukuliwe hatua za kisheria

"Naishukuru familia ya marehemu kwa kugoma kubomoa nyumba za wananchi hawa ,Namuagiza Mkuu wa Wilaya kufuatilia kwa karibu ili wakishakubaliana watu hawa wafanyiwe mpango wa kupewa hati za umiliki,"alibainisha Kunenge.

Licha ya maagizo hayo ,pia atafanya kikao na baadhi ya wawakilishi wa wananchi, msimamizi wa mirathi,familia na Mkuu wa Wilaya ili kuona namna ambavyo wananchi hao watalipa kwa utaratibu maalum na wenye kufaa.

Alisema ,baada ya utaratibu huo kukamilika wananchi hao watapata huduma muhimu ikiwa ni pamoja na maji na umeme huku akiwasisitiza wananchi kufuata sheria na taratibu pale wanapotaka kununua na hata kujenga nyumba zao.

Vilevile Kunenge alieleza,jambo ambalo limeamriwa na Mahakama hakuna anayeweza kutengua wala kuingilia isipokuwa hatua nyingine ya Kimahakama(Rufaa) na kwamba kinachotakiwa ni utekelezaji wa Mahakama .

Aliongezea, Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ipo katika kuwasaidia wananchi na ndio maana amefika eneo hilo kutatua mgogoro huo kwa kuzingatia taratibu na misingi ya kisheria.

Nae msimamizi wa mirathi ,Salim Mgombeo,alielezea anachotaka waliogoma kulipa waondoke lakini waliokubali kulipa wabaki na kwamba mgogoro huo ni mkubwa.

Baadhi ya Wananchi hao, akiwemo Amina Azizi na Hassan Ng'anzi,wanasema wapo tayari kulipa na wameomba Serikali iweke utaratibu maalum ambao utawawezesha kulipa bila usumbufu .



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...