Na  Khadija Kalili Kibaha

Wakongwe wa siasa nchini  Tanzania wamemzungumza na kummwagia sifa aliyekuwa  Rais wa Awamu ya Kwanza Hayati Julius Kambarege Nyerere  ikiwa ni katika kuadhimisha miaka 100 ya kuzaliwa kwake katika mdahalo uliofanyika kwenye Shule ya Siasa ya Mwalimu Nyerere iliyopo Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani.

Baadhi ya viongozi waliodadavua sifa za Hayati Nyerere ni pamoja na  Joseph Butiku ambaye aliwahi kufanya kazi na Hayati Nyerere ambapo alisema kuwa  alikua ni mtu mwenye maadili  na aliishia kwa utaratibu pia alipoanzisha Chama Cha TANU aliweka utaratibu hivyo ni wajibu wa watu wote kuishi  katika misingi ya kuwa na utaratibu.

Mkongwe Ally Mzee Ally kutoka Zanzibar alimwelezea Mwalimu Nyerere kuwa alikua ni muumini wa umoja jambo ambalo alilitilia msisitizi mwaka 1957 ambapo ndipo walupokutana na aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar Hayati Abeid Karume.
 
" kwa wakati huo alikua akiongoza Chama Cha Afro Shiraz ambapo Mwalimu Nyerere alichangia sana kuleta ukombozi  wa Zanzibar hivyo wakafanya majadiliano na kukubaliana kuanzisha muungano na kuunda nchi moja ya inayofahamika wa jina la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo Kila mtanzania aelewe kuwa chimbuko la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulianza mwaka 1957"alisema Ally

Wakongwe wengine waliozungumza ni pamoja na aliyewagi kuwa Waziri katika nyakati tofauti pia Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Bunda  Stephen Wassira, wengine waliozungumza ni pamoja na  aliyewahi kuwa Katibu Mkuu Joseph Butiku mstaafu ambaye alipata fursa ya kufanya kazi mbalimbali  na Hayati Nyerere  alisema kuwa Mwalimu  alikuwa mtenda  haki ambaye alifundisha  watanzania kujitegemea na kujali utu wa kila mwananchi,pia alifundisha ujamaa na kujitegemea  binadamu wote ni sawa pamoja na kuandika Katiba ya Chama,alikuwa mtu mwenye maadili na aliishi kwa utaratibu huku alitaka watu wote watiitaratibu zote zilizowekwa.

"Amani yetu tuilinde tuitunze tupinge ubaguzi ukabila ,udini  tuwe wamoja kwani hizi ndizo nguzo  kuu za amani kwani endapo hizi hazitakuwepo basi nchi haitakuwa na amani" alisema Ally.
 
Aliendelea kwa kusema kuwa "Nimezungumza  juu ya Imani ya Mwalimu Nyerere kuwa viongozi hatuwezi  kwenda mbele kama hatutafuata misingi ya haki kama Katiba  inachezwa itazaa rushwa, matapeli na machafu mengi yatazalishwa hivyo nawashauri viongozi wa leo muachane na mambo ya ubaguzi kwani Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi moja.
 
Kanali Mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania Simba Kalia alimwelezea Mwalimu Nyerere kuwa alikuwa na maoni katika nyanja ya uchumi Barani Afrika huku akiwa na mani kwamba bila ya Afrika kuungana haitaendelea kwani Afrika Ina kilakitu ikiwemo malighafi zote zinazogitajika katika kuitengeneza bidhaa mbalimbali duniani.
 
"Mwalimu aliamini katika kujenga uchumi wa viwanda Barani Afrika huku akiwa na maono ya kuwa siku moja nchi yetu itakuwa nchi ya Viwanda huku utekelezwaji wake ulianza kabla ya nchi kupata uhuru"alisema Kanali Mstaafu Simba Kalia.

Aliongeza kwa kusema kuwa  katika enzi zake za ujana alikuwa miongoni mwa vijana waliopata mafunzo ya kiteknolojia katika nchi mbalimbali akiwa kama mwanajeshi katika Shirika la Nyumbu lililoasisiwa na Mwalimu waliweza kuunda vipuri vya magari ya aina mbalimbali.

"Mwalimu ameondoka huku akiwa ameacha Taasisi na mifumo ambayo endapo tutawarithisha  vijana  vijana taifa letu litakwenda mbele"alisema Kanali Mstaafu Simba Kalia.
 
"Chini ya Uongozi wa Mwalimu Nyerere alifanya mambo makubwa kwa taifa ikiwemo kuanzishwa kwa kituo Cha Nyumbu,Mimi. nilikua mwizi mzuri sana wa teknolojia pia Niko tayari endapo nitapatiwa fursa ya kuwafundisha vijana wetu hasa wale wanaopita katika Jeshi la Kujenga Taifa JKT kwa sababu Nyumbu Kuna karakana za kuitengeneza magari ikiwemo  vipuri vya  treni ya Mwendokasi ambapo ujenzi wa reli yake unaendelea.

 Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Mzee Joseph Butiku akimvisha Katibu Mtendaji wa Chama Cha Mapinduzi Mstaafu na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mstaafu Mzee Pius Msekwa (kulia) beji ya Maadhimisho ya Miaka 100 ya Mwalimu Julius Nyerere wakati wa Mdahalo wa Kitaifa wa kuadhimisha miaka 100 ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uliofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha mkoani Pwani leo Aprili 9, 2022. (Picha na Adam Mzee)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...