Na Humphrey Shao,Michuzi TV

Wito umetolewa Kwa Watanzania na Kenya kuongeza mahusiano ya kitaaluma bila kuangalia tofauti zao za Mipaka ya nchi zilizomo katika jumuiya ya Afrika Mashariki.

Wito huo umetolewa hivi Karibuni na Naibu Mkuu wa Tasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) ,Prof Patrick Nsimama wakati wa hafla ya kuwaaga wanafunzi 24 waliokuja kujifunza katika Chuo hicho kupitia mradi wa RAFIC.

Prof. Nsimama ametaja kuwa licha ya nchi zetu kutenganishwa na Mipaka lakini Bado ni Moja Kwa maana ya Jumuiya na Bara Zima la Afrika.

"DIT Ndio Sehemu pekee ambayo kinajengwa kituo Cha umahiri Kwa ajili ya ICT Kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki, hivyo ni vyema Vijana na watumishi waliopo katika jumuiya kuja Tanzania kuchota maarifa yaliopo katika kituo hicho" Amesema Prof.Nsimama.

Aidha Amesema licha ya kuwa tofauti ya Mipaka Bado wanafunzi wetu wameonesha kuwa mitaala ya ufundishwaji hayatofautiani baina ya nchi na nchi, ndio maana wanafunzi hawa 24 kutoka Kenya wamefanya vizuri katika mafunzo yao.

Amesema wanafunzi hao wamjifunza Masuala ya Graphics Disigner ,Animation na Masuala ya Mtandao.

Naibu Mkuu wa Tasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) ,Prof Patrick Nsimama wakati wa hafla ya kuwaaga wanafunzi 24 waliokuja kujifunza katika Chuo hicho kupitia mradi wa RAFIC.

Mmoja wa Walimu kutoka Kenya walioongozana na wanafunzi kutoka Kenya akizungumza wakati wa hafla ya kutunukiwa vyeti wanafunzi 24 kutoka kenya

Dr.Garden Tesha akizungumza na Wanafuzni kutoka Kenya





Mratibu Radical na Mradi wa RAFIC ,Dr.Joseph Matiko akizungumza umuhimu wa mradi huo

Mmoja ya Wanafunzi kutoka Kenya akizungumza uzoefu wake katika Safari hii ya Mafunzo










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...