Na Amiri Kilagalila,Njombe
BAADHI ya wazee wa kijiji cha Itunduma kata ya Mtwango wilayani Njombe, wamechukizwa na kitendo cha vijana wa kijiji hicho kuacha nyumba na familia zao na kwenda kulala kwenye nyumba za wageni hali inayowapelekea kuwa na maswali mengi juu ya umuhimu wa nyumba hizo kwa wenyeji wa maeneo hayo.

Yenick Mwinami ni mmoja wa wazee wa kijiji hicho katika mkutano wa wananchi,idara ya dawati la jinsia na watoto walipokuwa wakitoa elimu juu ya unyanyasaji wa kijinsia,mauaji pamoja na udumavu ametumia nafasi hiyo kuhoji umuhimu wa nyumba hizo kwa wenyeji.

"Wenzetu wametujengea gesti huko,mimi ni mzee lakini,gesti Ile wamewajengea wenyeji au wamewajengea wageni"alihoji Bi.Yenick Mwinami

Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issah ametoa wito kwa jamii kurudi kwenye maadili na kuto acha nyumba zao.

"Cha msingi ni kwamba familia mrudi kwenye maadili,msiache familia na kukimbila gest,nyumba mmejenga kwa ajili ya familia zenu"alisema Hamis Issah

Vile vile amewatoa hofu wazee wa kijiji hicho na kudai kuwa nyumba hizo hujengwa sababu mbali ikiwemo wafanyabiashara na wageni wanaofika kwenye maeneo yao.

Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issah

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...