Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV
WANANCHI!!! Young Africans SC wameendeleza ubabe mbele ya Azam FC kwa kuchukua alama sita msimu huu wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara, baada ya kupata ushindi wa bao 2-1 katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es Salaam.
Wakiwa Viongozi wa Ligi hadi sasa, Yanga SC walipata ushindi huo wa bao 2-1, kwa mabao ya Wachezaji wake Djuma Shabani kwa mkwaju wa Penalti dakika ya 17 na bao la ushindi likifungwa na Mshambuliaji Fiston Mayele dakika ya 78 huku bao la Azam FC likifungwa na Rodgers Kola dakika za mwanzo za mchezo huo.
Yanga SC sasa wamejichimbia kileleni, wamejikusanyia alama 51 na michezo 19 huku Simba SC wakifuatia wakiwa na alama 37 michezo 17 na Azam FC wenye alama 28 na michezo 18 pekee.
Mchezo wa raundi ya kwanza wa Ligi Kuu, Yanga SC walishinda bao 2-0 katika uwanja wa Benjamin Mkapa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...