

Na WMJJWM- Dodoma
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula amekutana na Mwakilishi Mkaazi wa Umoja wa Mataifa (UN) Zlatan Millisic katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma Mei 18, 2022
Katika kikao hicho Dkt. Chaula na Mwakilishi Mkaazi wa UN Zlatan Millisic wamejadiliana masuala mbalimbali ikiwemo uwezeshaji Wanawake kiuchumi, Usawa wa Kijinsia na mapambano dhidi ya vitendo vya ukatili.
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum inaendelea kukutana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha inaweka mikakati ya Utekelezaji wa Sera na Mipango mbalimbali ya kutoa huduma kwa wananchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...