Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

KIKOSI cha Geita Gold FC kimekosa kiasi cha fedha Shilingi Milioni 30/- baada ya kupata sare ya bao 1-1 na Kikosi cha Simba SC katika mchezo wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara uliopigwa kwenye dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza.

Mkurugenzi wa Mji wa Geita, Mhe. Zahara Michuzi aliahidi kiasi hicho cha fedha endapo Kikosi cha Matajiri wa Dhahabu kikipata ushindi mbele ya Wekundu wa Msimbazi, Simba SC.

Geita Gold FC walianza kupata bao katika dakika ya 19 kupitia kwa Mshambuliaji wake kinara, George Enock Mpole baada ya Walinzi wa Simba SC kushindwa kuondoa mpira uliokuwa una zagaazagaa katika lango lao.

Dakika ya 25, Simba SC walisawazisha bao hilo kupitia kwa Mshambuliaji wao, Kibu Dennis Prosper baada kupiga Kichwa safi kilichowashinda Golikipa na Walinzi wa Geita FC na kujaa wavumi.

Baada ya mchezo huo, Geita Gold FC wanafika alama 35 na michezo yao 25 watabaki kwenye nafasi ya 5 ya msimamo wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara, wakati Simba SC wakibaki kwenye nafasi ya pili na alama zao 51 na michezo 25.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...