KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi Taifa ( CCM) Shaka Hamdu Shaka amewasili mkoani Manyara kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo amepokelewa na viongozi mbalimbali wa mkoa huo wakiongozwa na Katibu wa Chama hicho mkoa Naomi Kapambala.
Shaka ambaye ni Mlezi wa CCM Mkoa wa Manyara baada ya kuwasili na kupokelewa atapokea taarifa ya CCM Mkoa hasa inayoelezea hali ya Chama pamoja utekelezaji wa Ilani pamoja na taarifa ya Serikali Mkoa. Pia atatembelea miradi ya maendeo ambapo baadhi ya miradi imekamilika na mingine inaendelea.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...