
IGP Sirro amesema hayo leo wakati akifungua Mradi wa Kimkakati wa Fremu 12 za Maduka katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Kurasini Dar es salaam, Mradi ambao utawezesha chuo hicho kujiendesha kwenye mahitaji mbalimbali.
Kuhusu Usajili wa Pikipiki (Bodaboda) IGP Sirro amewataka wananchi hasa wanaonunua Pikipiki kwenye makampuni mbalimbali kuhakikisha wanafuata sheria za usajili kwa kuwa na kadi inayoonesha jina halisi la mmiliki wa chombo hicho.
Kuhusu maendeleo ya operesheni ya Panya Road IGP Sirro amesema kuwa, kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na Jeshi hilo kwa kushirikiana na vikundi vya ulinzi shirikishi imesaidia kudhibiti uhalifu unaotekelezwa na baadhi ya watu/vikundi vya watu na kwamba hadi sasa hali ya nchi ni salama.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...