Na.Abel Paul wa jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha
Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha kuanzia Mei 19 2022 linaendelea na operesheni maalumu ya kupambana na wahalifu wanaotumia Pikipiki maarufu kwa jina la “TATU MZUKA” ambapo wamekuwa kero kwa wananchi katika mkoa huu kwa siku za hivi karibuni.
Akitoa taarifa hiyo kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kamishina msaidizi wa Polisi ACP JUSTINE MASEJO amesema kuwa jumla ya watuhumiwa 14 walikamatwa katika operesheni hiyo kwa makosa ya kujihusisha na matukio mbalimbali katika jiji la Arusha, ikiwemo uporaji kwa kutumia pikipiki hizo maarufu tatu mzuka.
ACP Masejo amesema kuwa jumla ya pikipiki 12 zilikamatwa katika Operesheni hiyo huku mbili kati ya hizo zilikuwa hazina namba za usajili badala yake zilikuwa na plate namba iliyosomeka R.I.P SCOBER.
Ameendelea kusema kuwa Watumiwa hao wamehojiwa kwa kina na kukiri kufanya matukio ya uporaji, Pia amesema Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama linaendelea na operesheni kali ya kuwatafuta watuhumiwa wengine waliotajwa.
Kamanda Masejo ametoa wito kwa wananchi hususani wazazi na walezi kuwapa malezi mema vijana wao ili kuepusha kutojiingiza katika uhalifu vile vile niwaombe wananchi kuendelea kutoa taarifa za uhalifu kwa Jeshi la Polisi.
Home
HABARI
JESHI LA POLISI ARUSHA LAENDESHA OPERESHENI MAALUM KUPAMBANA NA WAHALIFU,YAWANASA 'TATU MZUKA' WALIOKUWA KERO KWA WANANCHI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...